• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

WAZAZI WAHIMIZWA KUWALINDA WATOTO DHIDI YA MITANDAO YA KIJAMII

Imewekwa : June 16th, 2023

Katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika Kijiji cha Rubao,  Kata ya Ijumbi Wilayani Muleba Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhe. Dkt Abel Nyamahanga amewahimiza wazazi kuhakikisha wanawalinda watoto kutojihusisha na mitandao ya kijamii ambayo inaweza kuharibu mienendo, tabia na maadili yao.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya amewaeleza wazazi kuwa kupitia kauli mbiu ya mwaka huu inayosema "Zingatia usalama wa mtoto katika ulimwengu wa kidigitali" ni vyema wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kuhakikisha kwamba usalama wa watoto unazingatiwa na kuwawekea mazingira salama yanayowazunguka hasa wanapokuwa wakiitumia mitandao ya kijamii.

"Sisi wazazi ni lazima tuwakinge watoto wetu wasijiingize kwenye mitandao hii ambayo inaweza ikaharibu tabia yao na  mwenendo wao kwa namna ambavyo watakuwa wakiitumia mitandao hiyo" amesema Mhe. Dkt Abel Nyamahanga.

Aidha,  amewahimiza wananchi kuacha matendo ya kiukatili hasa matendo ya mauaji ambayo yanasababisha watoto kubakia wakiwa yatima  jambo ambalo linapelekea watoto hao kutendewa vitendo ambavyo si rafiki kwa sababu ya kukosa wazazi wao.

Lakini pia amewahimiza wazazi kuwaruhusu watoto kushiriki katika mabaraza pamoja na michezo mbalimbali wawapo mashuleni jambo ambalo  litawasaidia kuwajengea uwezo wa kujiamini na kujieleza.

Sambamba na hayo amewahimiza Maafisa Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Dawati la Jinsia, Polisi, Walimu na Wadau wengine wote kuendelea kutoa huduma ya elimu ya malezi na makuzi ya watoto kwa wazazi na walezi ili waelewe wajibu wao wa kulea watoto katika msingi wa haki na usawa wa kijinsia.

Katika risala  iliyosomwa na Adiria Adronikus mmoja wa watoto walioshiriki maadhimisho hayo amesema kuwa kwa kipindi cha kuanzia july 2022 hadi april mwaka huu jumla ya vitendo vya kikatili 1,344 vimefanyika kwa watoto katika Wilaya ya Muleba ikiwemo ukatili wa kimwili, kihisia na wa kingono huku jumla ya wanafunzi 11 wakibainika kuwa na ujauzito wanafunzi 7 wakiwa wa shule ya Sekondari na wanafunzi 4 wakiwa wa shule ya msingi.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa