• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

WANANCHI WILAYANI MULEBA WAHIMIZWA KUWACHANJA MBWA NA PAKA MARA KWA MARA ILI KUWEZA KUWAKINGA DHIDI YA UGONJWA WA KICHAA CHA MBWA

Imewekwa : September 28th, 2023

Katika maadhimisho ya Siku ya Ugonjwa wa Kichaa cha Mbwa Duniani yaliyofanyika Kiwilaya katika Kata ya Muleba eneo la Uwanja wa Zimbihile na Uwanja wa Fatuma, wananchi wameendelea kuhimizwa kuchanja mbwa wao mara kwa mara kila baada ya mwaka ili kuwaepushia tatizo la kupata ugonjwa wa Kichaa cha mbwa.


Akizungumza kabla ya kutoa chanjo kwa baadhi ya Mbwa walioletwa na wananchi ili waweze kupatiwa chanjo hiyo wakiwa na uelewa wake, Bi. Joyce Kombe Daktari wa mifugo Wilayani Muleba, amewaelezea wananchi kuwa Ugonjwa wa Kichaa cha Mbwa ni ugonjwa hatari sana ambao unaweza kuambukizwa kwa mbwa na huyo mbwa akamuambukiza binadamu kwa kumng'ata jambo ambalo linaweza kuhatarisha maisha ya binadamu.


"Unaweza kumtambua mbwa mwenye dalili ya Kichaa pale ambapo utamuona mbwa wako alikuwa amezoea kuchangamka mara ghafla ukaona ameacha kuwa na hali hiyo au akawa mkali sana, akaanza kuwa na dalili za kung'ata vitu au ukamuona anaanza kutiririsha mate kutoka mdomoni, hizo ni baadhi ya dalili za mbwa mwenye virusi vya Kichaa cha mbwa" amesema Daktari Kombe.


Naye Ndg. Geofrey Kisai  ambaye ni Afisa Mifugo Kata ya Izigo ameongeza kwa kuwaeleza wananchi kuwa kama mwananchi mmoja akichanja mbwa wake  lakini jirani yake akawa na yeye ana mbwa ila hajachanjwa kuna uwezekano mkubwa wa mbwa huyo ambaye hajachanjwa akamuambukiza mbwa ambaye amechanjwa hivyo amewahimiza wananchi wote kuwa ni vema wakawa na desturi ya kuchanja mbwa wao mara kwa mara kila zoezi la chanjo linapofanyika.

Kwa upande wake  Siperatus Angelo mkazi wa Kata ya Muleba ameshauri kuwa ni vema wananchi wakawa wanawapeleka mbwa wao kupatiwa chanjo hata kwenye vituo vya afya ili kuweza kuwaepusha mbwa wao kupata maradhi ya kichaa cha mbwa.


Datius Kalinjuma Salvatory mkazi wa Kata ya Muleba ameeleza kuwa mbwa akichanjwa inasaidia kuishi kwa amani pamoja na wananchi wengine kwani mbwa akipata ukichaa kama hajachanjwa anaweza kumjeruhi mwanadamu na kumuambukiza ugonjwa wa ukichaa jambo ambalo linaweza kuleta athari katika jamii.


Katika maadhimisho hayo jumla ya mbwa 304 na paka 27 wamepatiwa chanjo ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa.


Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa