• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI NA MSINGI WAKABIDHIWA VISHIKWAMBI NA KUHIMIZWA KUVITUNZA KWA MATUMIZI ENDELEVU

Imewekwa : January 13th, 2023

Katika zoezi la kukabidhi vishikwambi Kwa walimu wa Shule za Sekondari na Shule za Msingi lililofanyika katika shule ya Sekondari Kaigara Wilayani Muleba Mwenyekiti wa  Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Mhe. Magongo Justus amewahimiza walimu kuvitunza vishikwambi hivyo na kuvitumia kwa matumizi sahihi yanayohusiana na Taaluma.

Akizungumza baada ya kukabidhi vishikwambi hivyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba amesema kuwa mwalimu anaruhusiwa kutumia picha za video vitini vya masomo alivyovichukua kutoka taasisi ya elimu ya Tanzania katika kishikwambi hicho kufundishia na kurahisisha utendaji wa kazi zao.

"Ni vema mkahakikisha mnavitunza vizuri vishikwambi hivi na sio lazima uende nacho kila mahali lakini wakati wa kazi unaweza ukakichukua ukakitumia katika kutekeleza majukumu yako" amesema Mhe. Magongo Justus.

Lakini pia amewasisitiza walimu  kuhakikisha wanasimamia taaaluma kwa bidii ili kuweza kuwasaidia wanafunzi kupata elimu bora na inayostahili ili kuweza kusaidia wanafunzi kuwa na ufaulu mzuri katika mitihani yao.

"Tunahitaji Mkuu wa matokeo sio Mkuu wa shule wa kukalia kiti tu na ndio maana nimesisitiza tunahitaji msimamie taaluma kwa kiwango kinachostahili ili wanafunzi waweze kupata elimu bora" ameongeza Mhe. Magongo Justus

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Ndg. Elias Kayandabila  amewasihi walimu kuvitunza vishikwambi katika mazingira salama ili visiweze kuibiwa kwa  kusudi la kuweza kusaidia katika utunzaji wa kumbukumbu na kurahisisha utendaji wa kazi zao.

 Katika risala iliyosomwa na Afisa Elimu Sekondari Ndg. Jared Muhile amesema kuwa Halmashauri imepokea jumla ya vishikwambi 2204 na kuelekeza vigawiwe Kwa Maafisa Elimu Ngazi zote za Halmashauri kata na walimu wote wa katika shule za msingi na Sekondari.

Aidha, amesema kuwa  endapo Mwalimu atakoma utumishi wa umma kwenye kada ya ualimu aidha kusitaafu kuacha kazi au kufariki au kuhama kada ya ualimu atalazimika kukabidhi kishikwambi hicho kwa mkuu wa kituo chake cha kazi na vishikwambi hivyo vitatumika kwa matumizi ya kujifunzia na kufundishia kwa walimu wa shule za msingi na Sekondari.

Mwalimu Charles Mkaluka kaimu Mkuu wa Shule ya Kiteme Sekondari amesema kuwa vishikwambi hivyo vitaweza kuwasaidia kuwarahisishia walimu kazi ya kupeluzi maswali na kupata mambo mengine mengi kama video na picha mbalimbali ambazo zinaweza kutumika katika kufundishia wanafunzi.

Naye Melines Maluka Afisa elimu kata wa Mayondwe ameeleza kuwa zoezi la ugawaji wa vishikwambi kwa walimu litazaa matunda makubwa naazuri katika uendeshaji wa zoezi la ufundishaji wa wanafunzi katika shule za Sekondari na shule za Msingi.

 Anord Rweyemamu Byabato Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Ruhanga ameeleza kuwa vishikwambi hivyo vitawarahisishia kazi ya utunzaji wa takwimu ambapo amesema kuwa hapo awali walikuwa wakitumia mafaili kutunza nyaraka na wakati mwingine nyaraka zilikuwa zinapotea lakini kwa kutumia vishikwambi hivyo vitaweza kuwarahisishia kazi hiyo.

Jumla ya Vishikwambi  2204 vimegawiwa kwa walimu ambapo Idara ya elimu Sekondari wamepokea jumla ya  vishikwambi 764 na shule za msingi wamepokea jumla ya  vishikwambi 1398 na maafisa elimu kata wamepokea jumla ya vishikwambi 42.

Imetolewa na:

kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa