• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

VIONGOZI WAHIMIZWA KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KUPAMBANA NA UVUVI HARAMU

Imewekwa : May 18th, 2023

Katika kikao kilichofanyika ndani ya ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhe. Dkt Abel Nyamahanga amewahimiza viongozi kuendelea kutoa ushirikiano wa pamoja na kulifanya zoezi la kupambana na uvuvi haramu kuwa endelevu ili kuweza kukomesha uvuvi haramu wilayani Muleba.

Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Wilaya amewahimiza Watendaji wa Kata, Watendaji wa Vijiji, Maafisa Uvuvi, Wenyeviti wa BMU, Wenyekiti wa Vijiji na Vitongoji kuhakikisha wanatenda kazi ya kupambana na uvuvi haramu kwa haki na kuhakikisha hawajihusishi na vitendo vya Rushwa ambavyo vinaweza kupelekea vitendo vya uvuvi haramu kuendelea kuwepo.

"Heshima ya kiongozi inakuja kutokana na namna unavyosimamia haki, tutende haki ibaki kutenda haki afadhari uhukumiwe usulubiwe kwa kutenda haki kuliko kusulubiwa kwa kutenda kwa ubadhirifu" amesema Mhe. Dkt Abel Nyamahanga.

Aidha ametoa onyo kwa viongozi ambao wanashiriki katika vitendo vya uvuvi haramu kuacha tabia hiyo kabla ya hatua kali za kisheria hazijachukuliwa dhidi yao.

Lakini pia amewaomba na kuwasihi wananchi wanaoshiriki katika vitendo vya uvuvi haramu kufanya shughuli zilizo harali na sio kwenye uvuvi haramu ili kuweza kulinda na kukuza mapato ya Halmashauri ambayo kwa asilimia 53 yanatokana na uvuvi.

 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Ndg. Jared Muhile  akizungumzia  pendekezo la kurudisha asilimia 5 za mapato yanayopatikana kutokana na uvuvi ili iweze kutumika katika zoezi la kupambana na  uvuvi haramu amesema kuwa watakaa na Mkuu wa Kitengo cha Uvuvi ili kuliweka kwenye mpango wa bajeti kwa lengo la kuhakikisha wanaondoa changamoto hiyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Bugasha Kata ya Mayondwe Ndg. Nathani Matungwa ameshauri kufungwa kwa mialo bubu ambayo haijasajiliwa inayotumiwa na wavuvi haramu jambo ambalo litasaidia kupunguza kasi ya uvuvi haramu.

Naye Mtendaji wa Kata ya Bumbire Marrygoreth Gelvazi amesema kuwa uvuvi haramu wa kutumia makokoro unahatarisha uwepo wa samaki ziwani na kuharibu mazalia ya samaki hivyo ameshauri kuendelea kufanyika zoezi la kupambana na uvuvi haramu ili kuweza kukomesha matumizi ya nyavu haramu.

Katika kikao cha kujadiri na kupanga mikakati ya kupambana na uvuvi haramu kilichofanyika tarehe 17/04/2023 na kuadhimia wavuvi wanaotumia nyavu haramu kurejesha nyavu haramu ndani ya siku saba,  zaidi ya dhana haramu  1229 zimerejeshwa zikiwemo timba 977, makila 85, makokoro 155 pamoja na mitumbwi 8.

 

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa