• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

SERIKALI YATOA KIASI CHA TSH MIL.584 KUJENGA SHULE MPYA YA SEKONDARI KATIKA KIJIJI CHA MAKONGORA KATA YA RUHANGA WILAYA YA MULEBA.

Imewekwa : January 8th, 2024

Kiasi cha Tshs Mil. 584 kimetolewa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kujenga Shule mpya ya Sekondari Makongora Katika Kata ya Ruhanga, itakayo kuwa na Vyumba nane vya Madarasa,Jengo la Utawala,Maabara tatu, Chumba cha komputa,Maktaba,Kichomea taka pamoja na matundu 20 ya vyoo.

Akiwasili katika eneo la ujenzi Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhe.Dkt.Abel Nyamahanga akiambatana na Mbunge wa Jimbo la Muleba Kaskazini Mhe.Charles Mwijage,Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bi.Christina Akyoo na baadhi ya Wataalamu wa Halmashauri(CMT)ambao waliungana pamoja kwenda katika kijiji hicho kukagua na kuona eneo la ujenzi wa Shule hiyo ambayo itakwenda kutatua adha ya wingi wa Wanafunzi ambao wanakwenda umbali mrefu kusoma katika Shule ya Sekondari Ruhanga.

Katika kikao kifupi kilichofanyika katika eneo la ujenzi wa Shule, Mhe.Dkt.Abel Nyamahanga  amewataka viongozi wa Serikali ya Mtaa na Wananchi wote kuhakikisha wanasimamia Mradi huo ipasavyo na kuhakikisha wanakuwa Walinzi wa Vifaa ambavyo vitaletwa kwa ajili ya ujenzi huo ambao ukikamilika utaifanya Shule hiyo kuwa bora na ya Mfano katika Wilaya ya Muleba.

Aidha Mhe.Dkt.Nyamahanga ameongeza kuwa ni muda muafaka sasa wa kutambua na kuweka mipaka ya kudumu katika eneo hilo kwa kulipima,na hivyo Mkurugenzi Mtendaji aliagizwa kuita wataalamu wa ardhi kupima na kutambua Mipaka ya eneo la Shule hiyo kabla ya watu kuingia ndani ya Mipaka ya eneo hilo.

"Mkurugenzi waite watu wa ardhi waje wapime eneo hili ili tutambue Mipaka yetu yakudumu kuwa inaishia wapi kwani kuna watu wataanza kuingia, hivyo tunataka Shule hii iwe nzuri ya mfano na ya viwango ili watu mjivunie na kuthamini kazi Nzuri inayofanywa na Mhe.Mbunge wetu, Diwani wetu, Chama na kazi Nzuri inayofanywa na Dkt. Samia Suluhu Hassan.”

Kwa upande wake nae Mbunge wa Jimbo la Muleba Kaskazini Mhe.Charles Mwijage alitumia muda huo kumshukuru Mhe. Nyamahanga,Mwenyekiti wa Halmashauri,Mkurugenzi Mtendaji pamoja na wataalamu kwa kukubali wazo la ujenzi wa Shule hiyo katika Kijiji cha Makongora  ambacho hakikuwa na shule hapo awali.

Imeandaliwa na kutolewa na;

Eusebius J. Kiluwa

KAIMU MKUU KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa