• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

SAMAKI WALIOVULIWA CHINI YA KIWANGO WAKAMATWA

Imewekwa : August 13th, 2021

Samaki aina ya Sangara kilo 400 wenye thamani ya fedha za kitanzania  TSH.4000,000 waliovuliwa chini ya kiwango cha sheria ya uvuvi Na. 22 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009 waliokuwa wakisafirishwa kutoka mwalo wa wa Ruhanga uliopo kata ya Magata Karutanga wilaya ya Muleba kuelekea wilaya ya Karagwe wamekamatwa leo Agost 13 majira ya saa 10 jioni na Mkuu wa wilaya ya Muleba, Mh. Toba Nguvila akiwa na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya.

Mkuu wa wilaya ameeleza kuwa hivi karibuni kamati ya ulinzi na usalama imeteua kikosi kazi kikijuisha wataaalamu wa sekta ya uvuvi kutoka ofisi ya Mkurugenzi na taasisi zingine za Serikali zinazosimamia shughuli za Ulinzi  na Usalama 

"Nawasihi sana wavuvi na wafanyabiashara kuacha mara moja biashara ya uvuvi haramu kwani Serikali ipo kazini na haita mvumilia mtu yeyote ambaye anajihusisha na shughuli za uvuvi haramu zinazosababisha uharibifu wa raslimali za taifa. Endapo samaki hawa wangevuliwa katika kiwango kinachostahiri wangekuwa na tani nyingi na tani hizo zingeingizia pato kubwa kwa taifa" ameeleza Mhe. Toba Nguvila.

Watuhumiwa waliokamatwa ni waendesha bodaboda watatu ambapo bodaboda wawili ni kutoka kijiji cha Rubya na kwa mujibu wa watuhumiwa hawa wameeeleza kuwa wametumwa na wafanyabiashara kupeleka samaki hao.

Aidha, Mkuu wa wilaya ameeleza kuwa zoezi hilo litakuwa endelevu huku akiwataka viongozi waliopo mwambao wa ziwa Victoria kuendelea kutoa ushirikiano ili kudhibiti uvuvi haramu katika wilaya. Pia amewaonya waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda wanaotumika kusafirisha samaki zisizokidhi viwango kuacha kujihusisha na shughuli hiyo ya uvuvi haramu kwani wamekuwa chanzo cha kutorosha samaki hao kwenda nje ya Wilaya na hadi nje ya nchi.

Naye Afisa Uvuvi wa Wilaya ya Muleba Bw. Wilfred Tibendelana amesema wataendelea kudhibiti uvuvi haramu kwani hawatomfumbia macho mvuvi au mfanyabiashara yeyote atakayehusika na uvuvi haramu na kusababisha kushuka kwa mapato ya Halmashauri.

Watuhumiwa hao waliokamatwa watafikishwa Mahakamani na watashtakiwa kwa sheria za nchi zilizowekwa.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano, Halmashauri ya Wilaya ya Muleba



Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa