• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

RPC,AAGIZA WATENDAJI WA KATA KUSHIRIKIANA NA ASKARI KATIKA KATA ZAO KUPAMBANA NA VITENDO VYA MAUAJI WILAYANI MULEBA

Imewekwa : May 9th, 2023

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kagera William Mwampaghale amewaagiza Watendaji Kata kushirikiana na Askari wa Kata kuwaelimisha wananchi kuacha vitendo vya kujichukulia sheria mkononi ili kuweza kupunguza vitendo vya mauaji Wilayani Muleba.

Akizungumza katika Kikao hicho kilichofanyika ndani ya ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kagera amewahimiza Watendaji wa Kata kuwashirikisha viongozi wa Kimira pamoja na viongozi wa Kidini kutoa elimu kwa wananchi ili vitendo vya mauaji viweze kukomeshwa Wilayani Muleba.

"Mnavyoenda kufanya mikutano kwenye maeneo yenu washirikisheni  na viongozi wa Kimira kiongozi wa kimira atatoa elimu hata kwa kilugha wananchi watamuelewa jambo ambalo linaweza kusaidia kwa wananchi hawa kuacha kuuana" amesema William Mwampaghale.

Lakini pia  amewaagiza maafisa mifugo kutoa elimu kwa wafugaji kufuga kisasa kwa kuhakikisha kiwango cha mifugo waliyonayo inaendana na eneo la ufugaji lililopo ili kuweza kupunguza migogoro ya wafugaji na wakulima.

Sambamba na hayo amewahimiza wafugaji kuhakikisha wanawaajiri wachungaji wa mifugo na walinzi wa mifugo yao wanaowafahamu pamoja na  kuhakikisha wanajenga mazizi yanayofaa kufugia mifugo yao ili kuweza kupunguza tatizo la wizi wa mifugo.

Wakati wa Ufunguzi wa Kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhe. Dkt Abel Nyamahanga ameeleza kuwa migogoro ya ardhi imekuwa chanzo cha mauaji pamoja na imani za kishirikina hivyo ameshauri kuwa ni vema wananchi wakawa wavumilivu wakaacha vitendo vya kujichukulia sheria mkononi pamoja na kuheshimu utawala wa sheria ili kuweza kuondokana na vitendo vya mauaji Wilayani Muleba.

Naye Mkuu wa Sehemu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Ndg. Charles Ntaki Mayunga ameeleza kuwa mfugaji anapopeleka mifugo yake kuuza kwenye mnada ni lazima awe na barua ya utamburisho kutoka kwa Mtendaji wa Kata au Mtendaji wa Kijiji kama mamlaka ambazo zinatambulika kusimamia ulinzi na usalama katika eneo husika na mmuzi akishanunua mifugo lazima atapewa kibari ambacho atakitumia mpaka sehemu anayopeleka mifugo hiyo.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kagera ameeleza kuwa kwa mwaka jana yameripotiwa mauaji ya watu 16 kwa Wilaya ya Muleba na kwa mwaka huu kuanzia mwezi wa kwanza hadi sasa tayari yameripotiwa mauaji ya watu 15 na kwa wizi wa mifugo mwaka jana yarilipotiwa matukio 15 na kwa mwaka huu tayari yameripotiwa matukio 30.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa