• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

NMB YAWAFIKIA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM, SHULE YA MSINGI KAIGARA-MULEBA

Imewekwa : August 11th, 2022

Benki ya NMB ni miongoni mwa wadau wa maendeleo ambao wamekuwa wakishirikiana na jamii na wakiunga mkono juhudi za maendeleo kwa kutoa mahitaji mbalimbali hususani sekta ya Elimu. Ambapo wamekabidhi vitanda 80 na magodoro 160 yenye thamani ya Tsh. 27.6 kwa Halmashauri ya Wilya ya Muleba kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum shule ya msingi Kaigara.

Akiwapongeza wakati wa hafla ya kukabidhi vitanda 80 (double decker) na magodoro 160, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Magongo Justus ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, iliyofanyika shule ya msingi Kaigara, ameishukuru benki ya NMB kwakuwa mdau mkubwa wa kuchangia shughuli maendeleo na kuwasihi kutochoka kujitoa kwa ajili ya jamii kwani bado kuna uhitaji mkubwa.

“Ninayo furaha kubwa sana asubuhi ya leo kuwa mgeni rasmi nyumbani, ambapo tunapokea ufadhili mkubwa sana kutoka benki ya NMB, nianze kwa kusema neno sana asanteni. Uwepo wa kituo hiki si kwa bahati mbaya ni kwasababu Serikali inatambua uhai na ustawi wa kila mtu, kumekuwepo baadhi ya tabia ya wazazi akishajaliwa zawadi ya mtoto ambae anamahitaji maalum asilimia kubwa wamekuwa wakiwaficha watoto hao. Serikali kwa kugundua hilo kukawepo sera na miongozo ya kuhakikisha watoto hawa wana haki ya kupata elimu, kuishi na kuwajali”, ameeleza Mhe. Magongo

Aidha, ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inaweka mipango thabiti ya kuhakikisha inamfikia kila mmoja na kwa mahitaji yake. Hivyo tukio hili litufanye kuwa mabalozi popote pale tunapojua kuna watoto wenye uhitaji maalum na wamefichwa ndani tuwabaini na kuhakikisha wanaletwa katika vituo/shule zinazotoa elimu kwa watoto hawa.

Kwa upande wake Meneja wa Kanda wa NMB, Ndg. Baraka Ladislaus kwa ameipongeza Serikali kwa kuboresha sekta ya elimu ikiwemo miundombinu ya kujifunzia na elimu bure ambapo Serikali imeongeza wigo wa kuwalipia wanafunzi wa kidato cha tano na sita ada ya masomo. Na wao kama wadau wanao wajibu wa kuunga juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali, kwa kuisaidia jamii kwani jamii ndio imeifanya benki hiyo kuwa kubwa kuliko benki zote Tanzania.

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa