• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

"NI LAZIMA IFIKE HATUA SISI KAMA VIONGOZI NA NINYI WANANCHI TUCHUKUE HATUA KWA PAMOJA KUTOKOMEZA UVUVI HARAMU" DC NGUVILA

Imewekwa : May 21st, 2022

Katika zoezi la kupambana na uvuvi Haramu Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila pamoja na Kamati ya Usalama wamefanya oparesheni ya kuchoma dhana za uvuvi haramu Katika kata saba wilayani Muleba zenye dhamani ya Tsh. Milioni 137.3.

Akizungumza katika zoezi hilo Mkuu wa wilaya amewaomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa ili kuweza kuwabaini na kuwakamata wale ambao hawajasalimisha dhana haramu ili hatua kali za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

"Tumejipanga kutokomeza uvuvi haramu tumejipanga kuendeleza uvuvi endelevu uvuvi haramu ni lazima tuupinge, uvuvi haramu ni lazima tuukatae kwa faida za kizazi hiki tusipofanya hivi hali itakuwa mbaya afya zitakuwa mbaya vijana wetu watakosa lishe, hata masoko ya samaki  hayatakuwa na faida" amesema Mhe Toba Nguvila.

Aidha, Amesistiza mitumbwi yote kutia nanga kwenye maeneo ya BMU na hata wanapokwenda kuvua lazima mitumbwi yote itoke kwenye maeneo ya BMU na kama kuna mitumbwi haijasajiliwa ni lazima isajiliwe kwa kusema kuwa mitumbwi ambayo haijasajiliwa ndio mabingwa wa uvuvi haramu.

Katika zoezi hilo amemsimamisha Mwenyekiti wa BMU Mwalo wa Nyakigera, Kijiji Kiziramuyaga, Kata ya Magarini Ndg. Charles Magadula baada ya kubainika kuwa miongoni mwa watu wanaomiliki  dhana haramu za kuvulia samaki katika kata hiyo.

Kwa upande wake Afisa Uvuvi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Ndg. Donatus Dominick amewaomba wananchi kwa kushirikiana na viongozi wasaidie kuunga mkono kutokomeza uvuvi haramu ili kumaliza suara la uvuvi haramu kwenye ziwa Victoria.

Naye Kaimu Afisa Uvuvi wa Halmashauri ya wilaya ya Muleba. Ignasio Rwina  amewaomba wananchi pamoja na wadau wa uvuvi kutoa ushirikiano kwa kumuunga Mkono Mkuu wa wilaya pamoja na kamati yake ya usalama ili kuhakikisha uvuvi haramu unakomeshwa katika wilaya ya Muleba.

Sayakulu Suleiman Ismail ameomba viongozi waendelee kudhibiti uvuvi haramu na kwa wale wanaojihusisaha na uvuvi halamu tutoe ushirikiano ili waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Humaru Amos Rwaikondo Mkazi wa kijiji Misikilo Kata Gwanseli ameeleza kuwa kwa wale ambao bado wamebaki na dhana haramu ni vema wasalimishe dhana hizo haraka kabla ya hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi yao na kuhaidi kutoa ushirikiano kuwabaini ambao bado watakuwa wameficha nyavu zao haramu.

Zeozi hilo la uteketezaji wa Nyavu haramu ambazo zimesalimishwa na wwnanchi limefanyika katika kata saba ambazo ni Kata ya Kata ya Kimwani, Kata ya Nyakabango, Kata ya Rulanda, Kata ya Gwanseli, Kata ya Izigo, Kata ya Katoke pamoja na Kata ya Mayondwe na Kuteketeza dhana zenye dhamani ya Tsh. Milioni 137.3.

Imeandaliwa na Kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA KUTWA KIDATO CHA KWANZA December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WATOA HUDUMA ZA AFYA WAHIMIZWA KUTOA HUDUMA BORA KWA WAGONJWA-DR MAGEMBE

    June 27, 2022
  • ZANA HARAMU ZA UVUVI ZAENDELEA KUTEKETEZWA MULEBA

    June 23, 2022
  • DC NGUVILA ATEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA USAMBAZAJI WA UMEME WA REA MULEBA

    June 22, 2022
  • MGOGORO WA ARDHI KIJIJI ILEMELA WATATULIWA

    June 21, 2022
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu: +255-756-350-183

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa