• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA APONGEZA KWA HATUA ZILIZOFIKIWA KATIKA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA

Imewekwa : November 30th, 2022

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Mhe. Magongo Justus ametoa pongezi kwa kamati za shule ambazo zimekamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa na kusisitiza kwa shule ambazo hazijakamikisha, kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa vyumba hivyo kwa wakati.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa vyumba hivyo, amewasisitiza walimu kuendelea kujituma na kuhakikisha wanasimamia vizuri ujenzi wa vyumba hivyo vya madarasa kwa umakini. Pamoja na kuwasisitiza Madiwani kuendelea kutoa elimu na kuwahamasisha wananchi katika mikutano ya Kata na Vijiji kujitoa katika uchangiaji wa shughuli za maendeleo

"Sio kwamba uchangiaji wa shughuli za maendeleo umeisha, ni vema tukaendelea kujitoa katika uchangiaji wa shughuli za maendeleo maana sio madarasa tu bado tuna na upungufu wa vyoo na maboma ambayo yanatakiwa yakamilke ili kuondoa uhaba wa miundombinu katika Wilaya yetu", amesema Mhe. Magongo

Aidha, ameshauri kuanzishwa kwa utaratibu wa kuvuna maji ya mvua kwa kujenga matenki katika ili maji hayo yaweze kusaidia katika shughuli mbalimbali zinazofanyika shuleni.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Ndg. Elias Kayandabila ameshauri walimu kufanya mpango wa kuweka mbao kwenye kuta ambazo zinaweza kutumika kama vizuizi vya kulinda kuta ili kuepusha kuta kuharibiwa na viti vya wanafunzi wanaokaa karibia na kuta

Naye Diwani wa Kata ya Ikondo Mhe. Venanti Mugolozi ametoa pongezi kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa kutoa kiasi cha Tsh. Milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa katika Shule ya Sekondari ya Kamishango jambo ambalo litasaidia  kupunguza changamoto ya uhaba wa vyumba vya madarasa katika shule hiyo

Shule zilizotembelewa na kukaguliwa ni pamoja na shule ya Sekondari Bureza vyumba vitatu vya madarasa,shule ya Sekondari Bujumba vyumba sita vya madarasa,shule ya Sekondari Bulembo vyumba viwili vya madarasa,shule ya Sekondari Ruhanga vyumba vitatu vya madarasa,shule ya Sekondari Rukindo vyumba vinne vya madarasa,shule ya Sekondari Rulama vyumba sita vya madarasa,shule ya Sekondari Kishuro vyumba vitatu vya madarasa,shule ya Sekondari Nshamba vyumba vinne vya madarasa na shule ya Sekondari Kamishango.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.



Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa