• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MWENYEKITI AWASIHI WALIOSAINI MIKATABA YA UKUSANYAJI MAPATO NA UDEREVA KUFANYA KAZI KWA NIDHAMU NA UTII

Imewekwa : February 1st, 2022

Katika zoezi la utiaji saini wa mikataba ya wakusanya mapato wa madereva lililofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Muleba Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Magongo Justus amewasihi waliosaini mikataba hiyo kufanya kazi kwa nidhamu, juhudi, weledi na utu ili waweze kufanya kazi yao kwa ufanisi.

Akizungumza katika zoezi hilo Mwenyekiti wa Halmashauri amewaeleza kuwa kazi hizo zinahitaji jitihada binafsi ambapo amewambia kuwa kama hawatakuwa na bidii maana yake kazi yao hawataweza kuifanya kwa ufanisi na wakishindwa kufanya kwa ufanisi basi watasimamishwa kazi hizo.

Sambamba na hayo Mwenyekiti amewaomba wakusanya mapato kuwaheshimu watu wote watakao kutana nao kwenye vituo vyao vya kazi kwa kuwambia kuwa umoja wao wa kuwaheshimu watu ndipo Halmashauri itasimama na kila mtu akajisikia vizuri kuishi katika Halmashauri ya wilaya ya Muleba.

"Unapokuwa na Heshima inakubeba na ikikubeba itakufikisha unako kwenda kwa kuheshimu kazi yako heshimu na aliyekusimamia ili kazi iwe ya manufaa na mafanikio makubwa kwako" amesema Mhe. Magongo Justus.

Lakini pia amewasihi waliosaini mikataba ya ukusanyaji wa mapato kuepuka tamaa za kutaka kutorosha mapato kwa kuwaeleza kuwa wakifanya hivo watakuwa wanazitia hatarini kazi zao na hiyo inaweza kuwapelekea kuchukuliwa hatua na kusimamishwa kazi zao.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Muleba Ndg. Elias Kayandabila amewasihi wakusanya mapato kwenda kutenda haki ili kinachotakiwa kupatikana kwa ajili ya Halmashauri kiweze kupatikana.

Na ameongeza kwa kuwaeleza kuwa umewekwa mda wa matazamio wa miezi mitatu ili kubaini kama kweli mtu ni mtiifu na atakayofundishwa na tabia zake vinaendana kwa kuwambia kuwa ndani ya miezi mitatu wataweza kuona kama mtu anafaa au hafai ili kama hafai iwape nafasi ya kumuuondoa.

Lakini pia amewambia kuwa kwa watakao kuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa maadili mwaka mzima ukiisha uwezekano wa kuwaongeza mda utakuwepo.

Naye Mwanasheria wa Halmashauri Ndg. Muyengi Muyengi amesema kuwa yeye kama mwanasheria atahakikisha kila anayekusanya mapato ya Halmashauri anakusanya kwa kuzingatia makubaliano na kwa atakayekiuka atakuwa mtu wa kwanza kusurutishwa kwa waaajili pamoja na vyombo vya Sheria na hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

Imeandaliwa na Kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 17-06-2025 June 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 07-05-2025 May 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa