• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MIRADI YOTE WILAYANI MULEBA

Imewekwa : August 8th, 2023

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Ndg. Abdalla Shaib Kaim ameridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyokaguliwa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2023

Akizungumza wakati wa kuzindua Mradi wa Maji Butembo, uliopo kata ya Bureza uliogharimu Tsh. milioni 986.9 Ndg. Abdalla Shaib Kaim amepongeza juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha ili kuwaletea maendeleo wananchi.

“Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 umefika katika mradi huu, umepokea taarifa ya mradi, ukakagua nyaraka na kisha kujionea kazi kubwa ambayo imefanyika. Ninayo kila sababu kuishukuru na kuipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa na nzuri inayoendelea kuifanya ikiwa ni pamoja na miradi mikubwa ya kimkakati kama mradi huu wa maji,” ameeleza Ndg. Abdalla Shaib

Aidha, ametoa salamu za Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa wananchi kuwa kupitia mradi huo wa maji wamesogezewa huduma ya maji safi na salama kwa nia na lengo la kumtua mama ndoo kichwani.

Bi. Nadhifa Yusuphu mkazi wa kijiji Butembo, kwa niaba ya wananchi wa Kijiji hicho na Kata ya Butembo ameshukuru Serikali kwa mradi huo ambao umekuwa mkombozi kwa wana Bureza kwani kwa miaka mingi walikuwa na changamoto ya kupata maji safi na salama lakini kupitia mradi huu wamepata maji safi na salama.

Mwenge wa Uhuru mwaka 2023, kwa Wilaya ya Muleba umekagua, umetembelea umeweka mawe ya msingi na kuzindua jumla ya miradi yenye thamani ya Tsh. bilioni 2.

Miradi iliyokaguliwa, kutembelewa, kuwekewa mawe ya msingi na kuzinduliwa ni Mradi wa uhifadhi wa mazingira kwa kupanda miti 500 shule ya Sekondari Nyakabango uliogharimu Tsh. milion 2, Mradi wa kikundi cha Vijana Tuinuane Seremala wenye thamani ya Tsh. milioni 32.5, Mradi wa barabara ya Shuriza-Usalama km 0.7 uliogharimu Tsh. milion 337.4.

Mradi wa Ukarabati na upanuzi wa Soko kuu Muleba Mjini uliogharimu Tsh. milioni 180.97, Mradi wa Jengo la Dharula Kituo cha Afya Kaigara uliogharimu kiasi cha Tsh. milioni 350 na Ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa shule ya Sekondari Bureza vilivyogharimu Tsh. milioni 60.

Aidha Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 umetembelea Ofisi ya Kijiji Kikuku iliyozinduliwa na mwenge wa Uhuru mwaka 2022 ili kuona uendelevu wa mradi huo uliogharimu Tsh. milioni 52.8. Pia Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 ulikagua shughuli za Mapambano dhidi ya Malaria, Mapambano dhidi VVU, Mapambano dhidi ya Rushwa, Mapambano dhidi ya Madawa ya Kulevya na Shughuli za Lishe.








Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa