• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MULEBA YAJIPANGA KUINUA HALI YA UFAULU KIDATO CHA NNE

Imewekwa : August 12th, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba katika Mkutano wake wa Baraza la Robo ya nne April-Juni, 2021/2022 kujadili taarifa za utekelezaji wa miradi ya maendeleo na shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Idara/Sehemu, imejipanga kuongeza hali ya ufaulu wa kidato cha nne kama ambavyo Wilaya inafanya vizuri katika ufaulu wa kidato cha sita.

Akizungumza kwenye Mkutano huo wa Baraza la Madiwani, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Magongo Justus Magongo ameeleza kuwa ni kweli iko haja ya kuwa na mikakati ya kupandisha hali ya ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi kidato cha nne ili matokeo yawe mazuri kama yalivyo matokeo ya kidato cha sita.

“Kama ambavyo mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini ameeleza, tunaipongeza Idara ya Elimu Sekondari kwa ufaulu wa kidato cha sita, wanafunzi wamefaulu vizuri, sasa ni wakati kuwa na mikakati na kuhakikisha ufaulu huu uwe na kwa kidato cha nne pia. Najua tukijipanga tunaweza”, ameeleza Mhe. Magongo.

Akitoa hoja hiyo, Mhe. Dr. Oscar Kikoyo, mbunge wa jimbo la Muleba Kusini ameipongeza idara ya Elimu Sekondari kwa ufaulu wa kidato cha sita na kueleza kuwa ufaulu wa daraja la kwanza ni asilimia 27, ufaulu wa daraja la pili ni asilimia 56.45, ufaulu wa daraja la tatu ni asilimia 16 na hakuna mwanafunzi aliyepata daraja la nne wala sifuri hivyo jitihada na nguvu kwa sasa ielekezwe kwa kidato cha nne. Na kueleza  namna wabunge walivyojipanga kuwapa motisha walimu kwa shule zinazofanya vizuri.

Naye Mhe. Charles Mwijage, mbunge wa Muleba Kaskazini ameeleza kuwa tayari ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa ajili ya kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2023 umeanza ikiwa sambamba na ujenzi wa shule mpya, huku akimtaka Mkurugenzi kujiandaa na umaliziaji wa maboma kwani fedha zote za mfuko wa jimbo zitakwenda kununua saruji kwa ajili ya ujenzi huo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Ndg. Evart Kagaruki alieleza kuwa ni jambo jema kuwa na mikakati ya kuinua ufaulu wa kidato cha nne. Hivyo suala hilo limepokelewa, wataalam watakaa na kuja na mikakati itakayowezesha kuinua kiwango cha ufaulu kwa kidato cha nne.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya la Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa