• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MULEBA YAENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA WATUMISHI

Imewekwa : August 11th, 2022

Katika jitihada za kuboresha mazingira ya watumishi, hususani walio katika mazingira magumu Halmashauri ya Wilaya ya Muleba kupitia Idara ya Elimu Msingi, imetoa pikipiki tatu kwa walimu wakuu wa shule za msingi Byengerere, Rutoro na Kyarutare zilizopo kata Rutoro kilometa 78 kutoka makao makuu ya Wilaya.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi pikipiki hizo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Mhe. Magongo Justus amesema kuwa Halmashauri inaendelea kuboresha mazingira ya watumishi kwa kuwapa motisha na kuwarahisishia katika majukumu yao ili waweze kutoa huduma stahiki.

“Ni matarajio yangu pikipiki hizi zitafanya kazi iliyokusudiwa sitarajii pikipiki hizi kwenda kufanya biashara ya kubeba abiria maarufu kama bodaboda. Ni vifaa vilivyonunuliwa kwa gharama kwahiyo utunzaji ni suala la msingi. Mwalimu utakayetumia utumie kwa malengo ya uendelevu ili zidumu”, ameeleza Mheshimiwa Magongo

Aidha, ameishukuru jamii ya wana Muleba, kwani kupitia ushuru unaokusanywa kwao umewezesha kununua pikipiki hizo. Ameendelea kueleza kuwa fedha ya mapato ya ndani inayokusanywa inafanya mambo makubwa kama hayo kwani wiki iliyopita zilikabidhiwa pikipiki tatu kwa maafisa mifugo wa kata za Kamachumu, Muhutwe na Kishanda. Na Halmashauri itaendelea kuboresha mazingira ya kazi ya watumishi kila mwaka kadri fedha inavyopatika.

Akiwasilisha taarifa fupi ya makabidhiano ya pikipiki hizo, Kaimu Afisa Elimu Awali na Msingi, Ndugu Titus Sudi Amour ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba kupitia Sehemu ya Elimu ya Awali na Elimu ya Msingi ilibaini changamoto ya usafiri kwa walimu wa shule za Msingi Kata ya Rutoro na kuona ipo haja ya kuwanunulia pikipiki zitakazowawezesha katika majukumu yao.

Aina ya pikipiki zilizonunuliwa ni Honda CC 125, zenye thamani ya jumla ya Tsh. milioni 10.5 sawa na Tsh. milion 3.5 kila moja pamoja na ongezeko la thamani (VAT). Na pikipiki hizo ni mali ya shule.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa