• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MKUU WA WILAYA YA MULEBA AWAOMBA WANANCHI WA MULEBA KUITUMIA WIKIYA SHERIA KUPATA MSAADA WA KISHERIA.

Imewekwa : January 24th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila katika siku ya uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria iliyofanyika katika mahakama ya wilaya amewaomba wanachi wa wilaya ya Muleba kuitumia wiki ya sheria ili waweze kupata msaaada wa kisheria ili kuweza kutatua chngamoto mbalimbali ambazo zinawasumbua kwa mda mrefu.

Akizungumza katika uzinduzi wa maadhimishi hayo amewasihi sana wananchi kwenda na kutoa ushirikiano wa kisheria kwa kupeleka shida zao za kisheria ili waweze kusaidiwa kwa kuwaeleza kuwa wapo baadhi ya watu wanadhurumiwa lakini kutokana na kutopata msaada wa kisheria lakini kama wangekuwa wanapata msaada wa kisheria huenda wasingekuwa wanadhurumiwa.

“Wiki hii itumike kama mkombozi wa maisha yetu, wiki hii itumike kama mkombozi katika kuhakikisha wananchi wetu wanapata haki, wiki hii itumike kama mwarobaini wa matatizo mbalimbali kwenye jamii yetu inawezekana na sisi wananchi tujitokeze tutumieni wakati huu ili kuweza kupata haki ili tunavofika kwenye kilele cha maadhimisho iwe ni tathmini ya yaliyofanyika kwenye wilaya” amesema Mhe. Toba Nguvila.

Lakini pia amewaomba mahakimu kuhakikisha wanatenda haki kwa kuwaeleza kuwa wasipotenda haki watakuwa hawaponyi Taifa kwasababu wakiamua tofauti na misingi ya haki maana yake mwananchi ataendelea kuumia kutafta haki yake ya msingi.

Ameongeza kwa Kumuomba Mhe.Asha Mwetinde  Hakimu Mfawidhi wa mahakama ya wilaya kuitumia hii wiki ya sheria kuwasaidia akina mama wajane na kumsisitiza kuhakikisha wanawahamasisha wananchi kushiriki katika wiki ya sheria ili waweze kutoa dukuduku zao kuweza kupata ushauri wa kisheria.

“Wajane wanateseka sana na mirathi jamii inafanya kuwadhurumu haki zao na wanadhurumiwa kwa sababu hawajui sheria unamkuta mjane anapoteza maisha kwa sababu ya masononeko na machungu ya kunyimwa haki” ameesema Mhe Mkuu wa wilaya.

Sambamba na hayo amewaomba wananchi kuitumia tovuti ya mahakama kusoma sheria ili kuweza kuwasaidia kuzijua sheria kupitia mtandao kwa kuwaeleza kuwa ziko  sheria nyingi zimewekwa kwenye tovuti ya mahakama.

Kwa Upande wake Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Muleba Mhe. Asha Mwetinde ameeleza kuwa watakuwa na siku saba  kwa ajili ya kuwafikia wananchi na jamii kwa ujumla katika sehemu zao ili kuwapa elimu juu ya sheria kwa kuwaeleza huduma zinazotolewa na Mahakama pamoja na maboresho yake yanayoendelea katika muhimili huo.

Lakini pia ameongeza kwa kusema kuwa itakuwa ni fursa kwa Mahakama ya Tanzania kupata mrejesho wa huduma zinazotolewa kwa maana ya maoni maralamiko mapendekezo kwa lengo la kuyapatia ufafanuzi utatuzi lakini pia kuyawekea mipango ya kuboresha ili kuleta tija kwenye huduma zinazotolewa na mahakama ya Tanzania.

Naye miongoni mwa wananchi waliohudhulia maadhimisho hayo  Ndg. Pastori Ihinduka amependekeza wazeee wa mabaraza ya kata wanapoteuliwa wapewe semina ya namna ya kuendesha mabaraza kwa haki.

Kauli Mbiu ya mwaka huu ni “Zama za Mapinduzi ya Nne ya viwanda safari ya maboresho kuelekea mahakama mtandao” Ikiwa na lengo la kuwasaidia wananchi kuweza kupata huduma za kisheria kimtandao kwa kuwasaidia wananchi kufungua kesi zao kwa njia ya kimtandao na kesi yake kuchakatwa kimtandao ili anayehusika aweze kupata taarifa bila yeye kufika mahakamani.

Imeandaliwa na Kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa