• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MKUU WA WILAYA AZINDUA RASMI UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA

Imewekwa : May 26th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila amezindua rasmi ujenzi wa Hospitali ya wilaya inayojengwa katika eneo la Marahala wilayani Muleba na kuwahimiza mafundi kujenga na kumaliza haraka ndani ya mwezi mmoja.

Akizungumza katika uzinduzi huo amesema kuwa kazi ya ujenzi wa hospitali ya wilaya ni lazima ifanyike usiku na mchana ili kumaliza haraka na kumuhimiza mhandisi kufika eneo la ujenzi kusimamia ubora wa ujenzi ambao unakidhi viwango

"Idadi ya mafundi hapa iongezeke mala dufu fundi mkuu ni lazima uajiri mafundi wengi wa kutosha ili kazi ifanyike usiku na mchana na vifaa visikosekane hatutaki kusikia kuna upungufu wa tofari kwa sababu fedha zipo kwenye akaunti anapofanya kazi hatua flani fundi alipwe fedha zake" amesema Mhe Toba Nguvila.

Aidha, Mkuu wa wilaya ameongeza kwa kusema kuwa wananchi wa Muleba wananenda kunufaika na ujenzi wa Hospitali ya wilaya kwa kueleza kuwa baada ya ujenzi kukamilika na hospitali kufunguliwa wananchi wataweza kupata huduma bora kwa uharaka na kwa unafuu na kuwasaidia kuwapunguzia gharama za matibabu ambazo walikuwa wanazitumia katika hospitali teule ya Rubya.

Sambamba na hayo ametoa shukrani kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa utoaji wa fedha za ujenzi wa hospitali ya wilaya kwa kutambua na kuona umuhimu mkubwa kwa wananchi wa wilaya ya Muleba kupata hospitali ya wilaya.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa wilaya ya Muleba Ndg. Greyson Mwengu ametoa pongezi kwa Mhe Rais kwa utoaji wa fedha za ujenzi wa hospitali hiyo na kuhaidi kuwa watasimamia kuhakikisha ujenzi unamalizika kwa wakati kwa kuzingatia ubora.

Naye Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi wilayani Muleba Ndg. Athuman Kahara ametoa shukrani kwa Mhe.Rais kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya wilaya na kuhaidi kuwa watahakikisha wanajenga kwa uharaka kama walivyojenga madarasa ya uviko 19 ili kumaliza kwa wakati.

Katibu Afya wa wilaya ya Muleba Ndg. Auxsilius  Mathew ameeleza kuwa wananchi walikuwa wanapata changamoto za matibabu kutokana na kutokuwepo kwa hospitali ya wilaya ambapo ameeleza kuwa wananchi walikuwa wanapata matibabu kwa gharama kubwa kwenye hospitali binafsi lakini ikishakamilika hospitali ya wilaya gharama zitakuwa ziko chini na wananchi wataweza kuzimudu.

Fedha zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya ni kiasi cha shilingi milioni 500 na majengo yatakayoanza kujengwa ni jengo la OPD kwa ajili ya wagonjwa wa nje na jengo la maabara ambapo majengo yote hayo mawili ndio yatajengwa kwa kiasi cha Tsh. Milioni 500

Imeandaliwa na Kutolewa na;

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa