• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MKUU WA WILAYA AWAAAGIZA VIONGOZI KATIKA KATA KUHAKIKISHA WANASIMAMIA NA KUPAMBANA NA UVUVI HARAMU

Imewekwa : May 12th, 2022

Katika ziara ya zoezi la kudhibiti uvuvi  haramu Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila amewaomba viongozi wakiwemo Watendaji wa Kata, Wenyekiti wa Vijiji na Vitongoji pamoja na viongozi wa BMU kuhakikisha wanadhibiti uvuvi haramu alipofanya ziara hiyo katika Kata ya Rulanda na Gwanseli wilayani Muleba.

Akizungumza katika ziara hiyo Mkuu wa wilaya ya Muleba ametoa onyo kwa viongozi  hao kuwa endapo ikibainika kwenye maeneo yao kuna wavuvi wanaotumia dhana haramu katika maeneo yao bila wao kutoa taarifa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

"Uvuvi wa kutumia timba makokoro, katuri, katwange, taa zenye mwanga mkali, boti na mitumbwi ambayo haijasajiliwa ni uvuvi ambao unaharibu ajira, ni uvuvi ambao unaharibu rasirimali za viwandani na ajira viwandani, ni uvuvi unaoharibu hata biashara za akina mama pamoja na kuikosesha mapato Halimashauri kwahiyo niwaombe kuacha uvuvi haramu" amesema Mhe Toba Nguvila.

Aidha, Mkuu wa wilaya amewaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa pale watakapokuwa wanaona shughuli za uvuvi haramu zikiendelea kufanyika katika ziwa ili kuweza kuwabaini na kuwachukulia hatua wale wote wanaohusika na vitendo hivyo.

Kwa upande wake Katibu tawala wa wilaya ya Muleba Ndg. Greyson Mwengu amewaeleza viongozi wa BMU wenyeviti wa vijiji na vitongoji na watendaji kuwa wakisimamia vizuri uvuvi haramu utakoma katika maeneo yao.

Lakini pia amewaomba viongozi hao kuwa na oparesheni zao za kufanya zoezi la kudhibiti uvuvi haramu kwa kuhakikisha wanatoa taarifa pale wanapobaini kuwa kuna uvuvi haramu katika maeneo yao ili kuweza kukomesha uvuvi haramu wilaya ya Muleba.

Naye Kaimu Afisa uvuvi wa wilaya ya Muleba Ndg. Ignasio Rwina amewaeleza wananchi kuwa kwa mujibu wa Sheria za uvuvi uvuvi wa kutumia  makokoro, timba na nyavu zenye macho madogo haviruhusiwi kutumika kuvua samaki na kuwaeleza kuwa nyavu zinazoruhusiwa ni kuanzia nchi sita kwenda juu hivyo amewaomba viongozi kutoa elimu kuwaelezea wananchi madhara ya dhana hizo .

Mkuu wa wilaya pamoja na kamati ya usalama amefanya ziara hiyo katika kata ya Rulanda na kata ya Gwanseli kijiji cha Misikilo.

Imeandaliwa na Kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa