• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MKANDARASI WA MRADI WA MAJI KYAMYORWA APEWA MDA WA MIEZI MITATU KUMALIZA MRADI

Imewekwa : January 11th, 2023

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhe. Kemirembe Rwota ametoa mda wa miezi mitatu kwa mkandarasi anayetekeleza mradi wa maji Kyamyorwa uliopo katika Kata ya Kasharunga Wilayani Muleba kukamirisha utekelezaji wa mradi huo ili wananchi waweze kupata huduma ya maji.

Akizungumza alipotembelea na kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo Kaimu Mkuu wa Wilaya amesema kuwa kwa fedha ipo ya kutekeleza na kukamilisha  mradi huo hakuna sababu yeyote ya kuongeza mda mrefu Wa kukamilisha mradi huo.

"Watu wa Kyamyorwa wanataka maji haraka iwezekanavyo fedha ipo kinachotakiwa sasa ni maji hivyo tunawaongeza miezi mitati tu ili mwezi wa tatu mama zetu na baba zetu wanaoishi eneo la Kyamyorwa waweze kupata maji na hili tunakwenda kulisimamia na tutahakikisha kazi inafanyika usiku na mchana ili mwezi wa tatu maji yaweze kupatikana" amesema Mhe. Kemirembe Rwota.

Aidha, Amewasihi wananchi kuhakikisha wanailinda miradi ya maji kwa kuhakikisha wanakuwa wazalendo  ili miradi hiyo  iweze kudumu na kutumika kwa mda mrefu kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

"Tunatakiwa kuwa wazalendo na kuwa na wivu na miradi inayoletwa kwenye maeneo yetu sisi ndio tuwe wa kwanza kuilinda sio tuanze kuiba na kuharibu miradi hii" amesema Mhe. Kemirembe Rwota.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kasharunga Mhe. Theobadi Kulandebe amemuomba Kaimu Mkuu wa Wilaya kwa wananchi waliopo karibia na eneo la tenki la maji lilipojengwa kuwekwa kwenye mpango wa kunufaika na huduma hiyo ya maji.

Aswida Athuman Mkazi wa Kyamyorwa ameeleza kuwa kupitia mradi huo utaweza kuwasaidia kuondokana na changamoto ya maji ambapo amesema kuwa hapo awali walikuwa wanategemea maji ya visima  maji ambayo msimu wa kiangazi yalikuwa yanakauka lakini kupitia mradi huu wanaimani wataweza kuondokana na changamoto hizo.

Naye Ester Nyanda ambaye pia ni mkazi wa Kyamyorwa amesema kuwa upatikanaji wa maji katika eneo hilo kwani hata maji yaliyopatikana kwa kuchimba yalikuwa hayatoshi kumudu mahitaji yao.

Mradi wa maji Kyamyorwa unatekelezwa kwa kiasi cha Tsh Bilioni 3.2 Kwa fedha za PFR na mpaka sasa mkandarasi anayetekeleza mradi huo amelipwa kiasi cha Tsh. Bilioni 1.2

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA KUTWA,BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM 2023 December 14, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA KUTWA KIDATO CHA KWANZA December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAKUSANYA MAPATO WAHIMIZWA KUFANYA KAZI YAO KWA UBORA NA KWA KIWANGO KINACHOSTAHILI

    February 01, 2023
  • MKUU WA WILAYA MTEULE WA WILAYA YA MULEBA AKABIDHIWA OFISI RASMI

    January 30, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KIASI CHA TSH. BILIONI 71.5 KUTUMIKA KATIKA MWAKA WA FEDHA 2023-2024

    January 24, 2023
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI NA MSINGI WAKABIDHIWA VISHIKWAMBI NA KUHIMIZWA KUVITUNZA KWA MATUMIZI ENDELEVU

    January 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu: +255-756-350-183

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa