• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MGOGORO WA MRADI WA MAJI BAINA YA KATA RULANDA NA BISHEKE WATATULIWA

Imewekwa : July 26th, 2022

Kutokana na mvutano uliokuwepo baina ya viongozi wa Kata ya Rulanda na viongozi wa Kata ya Bisheke uliotokana na mradi wa maji Kyamyorwa unaohudumia kata ya Kasharunga na Kata ya Rulanda, ambapo tanki la Kata ya Rulanda kujengwa katika kijiji cha Bisheke huku Bisheke ikiwa si mnufaika wa mradi huo, Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila amefika na kutatua mgogoro huo kwa kumuagiza Mkandarasi kujenga vituo vitatu vya kuchotea maji katika vitongoji vya Kata ya Bisheke vinavyopakana na eneo ambalo tanki la maji linajengwa.

Akizungumza mara baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili, ameeleza kuwa hakuna haja ya kuvutana maana miradi ya maendeleo ni ya waTanzania wote hivyo kumtaka Meneja wa Maji Vijijini kumuelekeza mkandarasi kujenga vituo vitatu vya kuchotea maji kwa kitongoji cha Ichwandimi, Kabuga na Nyakahanga vya kata ya Bisheke ili wananchi wa maeneo hayo nao wanufaike na mradi huo.

"Nimefika eneo la mradi na kujionea hali halisi, sioni sababu ya kuendelea kuvutana nakuagiza Meneja wa RUWASA, muelekeze Mkandarasi, vituo vitatu kati ya vituo kumi na tatu vinavyojengwa katika mradi huu vijengwe katika vitongoji vya Kijiji hiki mahali ambapo tanki la maji linajengwa. Haitakuwa busara tanki la maji linajengwa hapa Kata ya Bisheke lakini mradi unakwenda kuhudumia kata ya jirani ya Rulanda na wakati huohuo wananchi wa eneo hili wanahitaji huduma ya maji, hivyo vituo vitatu vya kuchotea maji vijengwe kata ya Bisheke na zile vituo 10 ndio vikahudumie kata ya Rulanda", ameeleza Mhe. Nguvila.

Aidha, ameagiza kuwa mama mwenye eneo  ambapo tanki la maji linajengwa alipwe fidia ya mazao yake yaliyoondolewa kupisha ujenzi wa tanki. Huku akielekeza mradi utakapokamilika bei ya ndoo ya maji isizidi shilingi 50 na kuwasisitiza wananchi kuwa mradi utakapokamilika wahakikishe wanaulinda mradi huo bila na si kufanya uharibifu.

Kwa upande wa Madiwani wa Kata ya Bisheke Mhe. Alexander Petro na Kata ya Rulanda Mhe. Evart Tiletwa wamemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kufika kuona hali halisi, kuzungumza na viongozi na kutoa maelekezo ambayo yameafikiwa na pande zote mbili huku jina la Mradi likibaki kama lilivyo Mradi wa maji Kyamyorwa.

Naye Mhandisi Kaiza Zephline Kaimu Meneja RUWASA Wilaya ya Muleba ameeleza kuwa mradi huo umetengewa bajeti ya kiasi cha Tsh. Bilioni 3.2 na mradi huo utatekelezwa na Mkandarasi Mbeso Engineering kutoka Dar es Salaam ulianza kutekelezwa tarehe 24/05/2022 na unatarajiwa kukamilika tarehe 25/11/2022.

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 17-06-2025 June 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 07-05-2025 May 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa