• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MGOGORO WA ARDHI KIJIJI ILEMELA WATATULIWA

Imewekwa : June 21st, 2022

Kamati ya uchunguzi wa migogoro ya ardhi imewasilisha taarifa ya uchunguzi wa mgogoro wa ardhi katika kijiji cha Ilemela, Kata ya Gwanseli, Wilaya ya Muleba kwa kuwabainisha wanaomiliki ardhi kihalali na wasiomiliki ardhi kihalali hivyo kutakiwa kuyarudisha maeneo waliyonayo kwa Serikali ya Kijiji.

Akizungumza katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho Mkuu wa Wilaya ya Muleba, Mhe. Toba Nguvila amewaeleza wananchi wa kijiji hicho kuwa hakuna ardhi ya kijiji itamilikiwa na mtu bila kufuata utaratibu ikiwemo kuitishwa kwa mkutano wa hadhara ili wananchi kuridhia na kama kuna mtu atamiliki ardhi kinyume na utaratibu huo hatua zitachukuliwa dhidi yake ikiwa ni pamoja na kunyanganywa eneo hilo.

"Kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi ya Vijiji ya mwaka 1999 maamuzi ya ardhi ya Kijiji ambayo inatakiwa kutumika kwa ajili ya shughuli fulani au kumilikiwa na mtu ni lazima Mkutano wa Kijiji ukae ufanye maamuzi na wanakijiji wasaini na kuwa na muhtasari kwa ajili ya rejea,” ameeleza Mhe. Nguvila

Aidha, amesisitiza kutengenezwa kwa mpango maalumu wa matumizi bora ya ardhi na kusisitiza ushiriki wa wananchi wote katika mpango huo ili wananchi wote waweze kufahamu ni mipango ipi imepangwa kwa ajili ya matumizi bora ya ardhi ya kijiji.

Sambamba na hayo amesema kuwa kwenye mpango wa matumizi bora ya ardhi utakaowekwa na kupitishwa kuwa eneo la njia ya mifugo ni marufuku mtu mwingine kuziba eneo hilo kwa sababu njia za mifugo zinapozibwa ndo chanzo cha migogoro ya wafugaji na wakulima.

Ripoti ya kamati ya uchunguzi iliyosomwa na Mchunguzi wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Muleba, Inspecta Joseph Dishon ameeleza kuwa vyanzo vya migogoro ya ardhi katika Kijiji cha Ilemela vimetokana na kutofuatwa kwa Sheria ya Ardhi ya mwaka 1999 hivyo ili kuondoa changamoto hizo kamati ilipendekeza yafuatayo:-

Serikali ya Kijiji itambue Maeneo yake na kuyawekea ulinzi ili kuepusha kuvamiwa na wananchi wenye uchu wa ardhi bila kufuata utaratibu na Serikali ya Kijiji imeombwa kuunda kamati maalumu ya kubainisha ardhi zilizorudishwa pamoja na ardhi ambazo umiliki wake haukuwa halali ili ziweze kuwekwa vizuri kwenye kumbukumbu ya ardhi ya kijiji pamoja na kuweka mipaka ya kudumu.

Lakini pia kwa waliojimilikisha ardhi kinyume na utaratibu warudishe ardhi hizo kwenye Serikali ya Kijiji na ardhi zitakazorudishwa zitambuliwe na Serikali ya Kijiji ili ziweze kuwekwa kwenye orodha ya ardhi wazi za kijiji.

Imetolewa na:

Kitengo cha Teknolojia ya Habari, Mawasiliano na Uhusiano

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa