• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MADIWANI WAAGIZWA KUTOA USHIRIKIANO KUPAMBANA NA UVUVI HARAMU KATIKA KATA ZAO

Imewekwa : November 17th, 2022

Katika Kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika lkatika ukumbi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Katibu Tawala wa Wilaya Ndg. Greyson Mwengu amewaagiza Madiwani kutoa ushirikiano katika maeneo yao ili uvuvi haramu uweze kutokomezwa.

Akizungumza katika Baraza hilo Katibu Tawala wa Wilaya ya Muleba amesema kuwa endapo viongozi watashindwa kusimamia na kupambana na uvuvi haramu jambo hilo litapelekea kuadimika kwa samaki katika Wilaya ya Muleba hivyo ni vema viongozi wakiwemo madiwani, watendaji wa kata na vijiji pamoja na wenyekiti wa vijiji kuhakikisha wanatoa ushirikiano kupambana na uvuvi haramu kuhakikisha unakomeshwa katika Wilaya ya Muleba.

"Kama unafanyika uvuvi haramu na kiongozi ukaonekana unautetea mwisho wa siku samaki wataisha yatabakia tu maji ya kuoga na kupikia na siku samamki wakiisha wananchi watayahamishia hayo madhambi kwako na kusema kuwa wewe kiongozi sio mzuri kama umishindwa kusimamia na kuhakikisha unapambana na uvuvi haramu" amesema Ndg. Greyson Mwengu.

Aidha. Katika Baraza hilo amewaomba  madiwani kuhakikisha wanasimamia kwa ukaribu sana ujenzi wa madarasa yanayojengwa kwa sasa katika maeneo yao ili madarasa hayo yaweze kukamila kwa wakati na kwa viwango vinavyostahili ili kufikia tarehe 25 madarasa yote yawe yamekamilika.

"Madiwani na nyie kwa nafasi yenu mpite katika hivyo vyumba vya madarasa mkague na kuelekeza kama sisi tunavyopita na kuelekeza na nyie fanyeni hivyo ili ujenzi wa madarasa uweze kukamilika kwa wakati uliopangwa" ameongeza Ndg. Greyson Mwengu.

Sambamba na hayo amewaagiza madiwani kuwahimiza wananchi  kuendelea kulima mazao ya chakula kwa kuweka akiba ya vyakula ili kuweza kukabiliana na janga la uhaba wa vyakula katika Wilaya ya Muleba.

Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Mhe. Muhaji Bushako amesema kuwa ni vyema madiwani wakahakikisha wanatoa ushirikiano wa kupata majina ya mialo ambayo inashiriki katika uvuvi haramu na kufika katika mialo hiyo kujionea ili hatua za kisheria ziweze  kuchukuliwa  kwa watu wanaofanya vitendo hivyo.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Ndg. Stewart Mtondwa amesema kuwa  kwa mtu atakayemuona mvuvi anayefanya uvuvi haramu kwa kutega samaki bila kutumia nyavu zinazostahili ni vizuri akatoa taarifa kwa uongozi wa Halmashauri na jeshi la polisi ili kuweza kunusuru na kukomesha uvuvi haramu.

"Hayo yote tukiyafanya kwa pamoja viongozi katika ngazi ya Kata, ngazi ya Tarafa na ngazi ya Wilaya wakiwemo pia waheshimiwa madiwani tunahitaji kushikiana kwa pamoja kuhakikisha uvuvi haramu unatokomezwa katika Wilaya yetu" amesema Ndg. Stewart Mtondwa.

Diwani wa Kata ya Biilabo  Mhe.  Beatus Mussa  ameshauri kwa kusema kuwa ni vema wananchi wakapanda mazao ya mda na kuhifadhi chakula ili chakula hicho kiweze kuwasaidia kupambana na uhaba wa chakula na hata kuwasaidia maeneo mengine ambayo yanaweza kukumbwa na changamoto hiyo.

Akizungumzia suara la uvuvi haramu amesema kuwa ni vyema kwa kata ambazo zinapakana na ziwa wahamasishe wananchi wao waweze kuachana kabisa na uvuvi haramu ambapo amesema kuwa uvuvi haramu unaharibu hata mazalia ya samaki jambo ambalo linaweza kuhatarisha uchumi wa uvuvi katika maeneo yetu.

Naye Pastory Gwanchele Diwani wa Kata ya Nyakabango ameeleza kuwa ni vema Maafisa uvuvi wakatoa elimu kwa wavuvi wadogo wadogo kuhusiana na madhara ya uvuvi haramu ili waweze kuachana na uvuvi haramu jambo ambalo litasaidia kupuguza uvuvi haramu Katika Wilaya ya Muleba.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa