• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

MAAFISA BIASHARA WASISITIZWA KUWATEMBELEA WAFANYABIASHARA KWENYE MAENEO WANAKOFANYIA BIASHARA ZAO

Imewekwa : January 11th, 2023

Katika Kikao cha Baraza la Wafanyabiashara kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhe. Kemirembe Rwota amewasihi maafisa Biashara kuwatembelea wafanyabiashara ili kubaini na kutatua changamoto walizonazo.

Akizungumza katika Kikao hicho Mkuu wa Wilaya  amesema kuwa ni vema Maafisa Biashara wasiishie kufanya kazi maofisini wafike hadi kwa wafanyabiashara ili waweze kujua changamoto zao na kumsisitiza Mkurugenzi kuhakikisha anafuatilia kujua kama hayo yanafanyika.

"Mnaweza mkawa mna desturi ya kuwatembelea wafanyabiashara lakini kama mnawatembelea mala moja kwa mwaka mnakuwa hamjatimiza majukumu hata kama wana changamoto zao wanataka kuwaelezea wanakosa pa kuwapata hivyo nadhani tutoke tuwatembelee wafanyabiashara mpaka kwenye maeneo wanakofanyia biashara zao" amesema Mhe. Kemirembe Rwota.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Ndg. Stewart K. Mtondwa amesema kuwa waendesha bodaboda kupata leseni ni kitu cha msingi sana ambacho kitawasaidia kuendesha shughuli zao ambapo ameeleza kuwa kama wakiwezeshwa wakapata leseni Halmashauri pia inaweza kupata mapato na biashara yao yao ya Bodaboda ikawa halali.

Naye, Afisa Biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Ndg. Dickson Mnyaga ameeleza kuwa kutokana na wananchi wa Wilaya ya Muleba kujishughulisha na shuguli za Kilimo,Uvuvi na Ufugaji malighafi zinazotokana na shughuli hizo ni kichocheo kikubwa cha kuanzisha viwanda mbalimbali  ndani ya wilaya ambapo mpaka sasa wilaya ina viwanda vya vya kati 64 vinavyochakata mazao ya kilimo ikiwa ni pamoja na viwanda vya kukoboa na kusaga kahawa, kukoboa na kusaga unga na kufungasha unga, kukoboa mpunga na kufungasha kwa madaraja.

Kanga Makusi meneja wa Benki ya NMB Muleba ameshauri kurasimisha shughuli ndogondogo zilizopo maeneo ya vijijini na mjini ambapo amesema kuwa wilaya ingeweza kuongeza mapato kama ingetafutwa namna nzuri ya kuwatambua na kuwawezesha wafanyabiashara wadogo wadogo.

Meneja wa TRA Daniel Makirikita Wilaya ya Muleba amesema kuwa sio wafanyabiashara wote wanaoitakiwa kuwa na mashine za EFD kwa wafanyabiashara wanaotakiwa kuwa na mashine za EFD kisheria mauzo yao yanatakiwa kuwa Tsh.  milioni 11 na kuendelea na wafanyabiashara wenye mauzo pungufu ya hapo wanatakiwa kuwa na kitabu cha kawaida cha kutoa lisiti kwa wateja.

Naye Khalfan Abubakari Mwenyekiti wa jumuiya ya Wafanyabiashara Wilayani Muleba amesema kuwa ili kuweza kufikia malengo ya makusanyo ya mapato ya Halmashauri ni vema ikatafutwa namna ya kuwakuza wafanyabiashara au kuanzisha biashara mpya au kutengeneza miradi mingine mipya ili kuweza kuyafikia malengo bila kuwaumiza wananchi.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA KUTWA,BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM 2023 December 14, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 27, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA KUTWA KIDATO CHA KWANZA December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAKUSANYA MAPATO WAHIMIZWA KUFANYA KAZI YAO KWA UBORA NA KWA KIWANGO KINACHOSTAHILI

    February 01, 2023
  • MKUU WA WILAYA MTEULE WA WILAYA YA MULEBA AKABIDHIWA OFISI RASMI

    January 30, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KIASI CHA TSH. BILIONI 71.5 KUTUMIKA KATIKA MWAKA WA FEDHA 2023-2024

    January 24, 2023
  • WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI NA MSINGI WAKABIDHIWA VISHIKWAMBI NA KUHIMIZWA KUVITUNZA KWA MATUMIZI ENDELEVU

    January 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu: +255-756-350-183

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa