• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

KIASI CHA TSHS BIL.1 KUTOLEWA NA SERIKALI ILI KUKAMILISHA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA YA MULEBA IFIKAPO JANUARI,2024.

Imewekwa : December 16th, 2023

Januari,2024 kiasi Cha shilingi Bil.1 kinatarajiwa kutolewa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuendeleza ujenzi wa majengo mengine mapya ya Hospitali ya Wilaya ya Muleba ambayo kwa sasa ukamilishaji wa ujenzi wa baadhi ya majengo unaendlea.

Akizungumza na Wananchi wa Wilaya ya Muleba Mhe.Mohamed Mchengerwa Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) amesema kuwa Serikali itatoa Kiasi Cha Shilingi Bil.1 ilikuongeza majengo mengine mapya katika Hospitali ya Wilaya ili kuwezesha huduma bora kwa Wananchi wa Wilaya ya Muleba.

"Wabunge wameomba sana kuhusiana na hili swala lakini nimelipeleka kwa Waziri Mkuu hivyo nimemwagiza Katibu Mkuu kuwa ifikapo mwezi Januari, 2024 Mhe.Rais amesema ataleta kiasi Cha Tshs Bil.1 kwa ajili ya ujenzi wa majengo mengine mapya ya Hospitali ya Wilaya."

Aidha Mhe.Mchengerwa amesema Serikali itaongeza vituo vya Afya vipya viwili ambavyo vitajengwa katika Wilaya ya Muleba huku kimoja kikitarajiwa kujengwa katika Jimbo la Muleba Kusini na kingine ambacho kinatarajiwa kujengwa katika Jimbo la Muleba Kaskazini.

"Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan anawapenda sana amesema atawaongezea kiasi kingine Cha fedha ili Kujenga vituo vya Afya viwili ambavyo vitajegwa katikaJimbo la Muleba Kaskazini na Jimbo la Muleba Kusini, lakini pia kwa Jografia ya Muleba nimemwagiza Katibu Mkuu kutafuta fedha nyingine ili tuongeze zahanati nyingine katika Wilaya ya Muleba na Wabunge wenu watachagua zijengwe wapi"

Sambamba na hilo Mhe.Mchengerwa ameongeza kuwa Serikali inatarajia kuleta Magari mawili ya wagonjwa yaani(Ambulance) na Boti ya kisasa (Fiber Boat) yakubebea wagonjwa(ambulance) ambazo zitasaidia kuboresha huduma ya Afya katika Jimbo la Muleba Kaskazini na Jimbo la Muleba Kusini.

"Mhe.Rais ameridhia na ameniambia ataleta gari mbili za wagonjwa na gari moja itapelekwa Muleba Kusini na gari Nyingne itapelekwa Muleba Kaskazini,lakini pia kule kwa kaka yangu Mwijage Mhe.Rais amesema ataleta Boti ya wagonjwa(ambulance) inayo kimbia kwa kasi zaidi kwenye maji"

Kwa upande wao wabunge wa Muleba(Kusini na Kaskazini) Mhe.Charles Mwijage na Mhe.Oscar Kikoyo walitumia muda huo kumshukuru na kumpongeza Mhe.Rais pamoja na Mhe.Mchengerwa kwa kazi kubwa wanayoifanya kwani Wilaya ya Muleba imeletewa Miradi Mingi Ikiwa ni pamoja na Miradi ya Afya, Shule, Maji pamoja na Miradi ya Barabara inayotekelezwa na Tarura.

Imetolewa na;

Kaimu Mkuu Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa