• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

KAMATI YA MAJI YAAGIZWA KUWEKA ULINZI KWENYE VYANZO VYA MAJI

Imewekwa : August 19th, 2021

Wakala wa Maji Vijijini RUWASA wilaya ya Muleba Mkoa wa Kagera imefanya ukarabati wa kawaida katika miradi mitatu mikubwa ya maji ambayo ni mradi wa maji Kasharunga uliopo kijiji Kasharunga, kata ya Kasharunga, mradi wa maji Ruteme uliopo kijiji Ruteme na mradi wa maji Kyota uliopo kijiji cha Kyota, Kata ya Kimwani.

Akikagua miradi hiyo Mkuu wa Wilaya ya Muleba, Mhe. Toba Nguvila ameagiza kamati zote za maji wilaya ya Muleba kuhakikisha wanawake walinzi kwenye vyanzo vya maji ili kulinda miundombinu ya maji na kuondoa madhara ya uharibifu wa vyanzo vya maji inayoweza kuathiri watumiaji maji.

"Serikali inatumia fedha nyingi sana kujenga na kuendeleza miradi hii, hivyo ni jukumu la wananchi kuitunza na kuendeleza kwa manufaa yao na vizazi vijavyo. Hivyo naagiza kuanzia sasa kila chanzo cha maji lazima kiwe na mlinzi ili kuepukana na changamoto ya kupotea kwa miundombinu ya maji ambayo inahujumiwa na watu ambao hawana nia njema na uwekezaji wa Serikali" ameeleza Mhe. Toba Nguvila. 

Maagizo hayo ameyatoa baada ya kutembelea miradi hiyo na kukuta katika miradi yote mitatu hakuna mlinzi hata mmoja kwenye vyanzo vya maji. Aidha, amezitaka kamati za maji mradi wa Rutema na Kyota kupunguza gharama za uuzaji maji kutoka shilingi 100 kwa ndoo moja hadi shilingi 50 kwa ndoo ili kila mwananchi aweze kutumia huduma hii muhimu ya maji kutokana na baadhi ya wananchi kuendelea kuchota maji katika mto kwa kukosa fedha za kununua maji kwa maelezo kuwa gharama zipo juu ya uwezo wao.

Kwa upande wa Meneja wa wakala wa usambazaji maji vijijini (RUWASA) Wilaya ya Muleba, Mhandisi Patrice Jerome ameeleza kuwa jukumu la kuweka walinzi na kupunguza gharama ya kuchota kwa kila mradi wa maji ni jukumu la kamati za maji zilizochaguliwa na jamii na kamati hizo zinajiendesha zenyewe hivyo wao kama wanasimamia maelekezo yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ili wananchi waweze kuondokana na adha hiyo na watumie maji kwa wingi kama Serikali ilivyowakusudia.

Wananchi wameishukuru Serikali kwa kuwaletea miradi hiyo ya maji ambayo kwa kiasi kikubwa imewaondolea changamoto ya kutembea umbali mrefu kufata huduma ya maji na kupata maji safi na salama.

Mradi wa maji Ruteme ukarabati uliofanyika ni kuweka mfumo wa sola kutoka nishati ya kutumia mafuta ya dizeli, kujenga uzio katika chanzo cha maji ambao umegharimu Tsh. 75,000,000. Mradi wa maji Kyota, ukarabati uliofanyika ni kurudisha mota na pampu zilizoharibika zilizogharimu Tsh. 30,000,000 na mradi huu unahudumia vijiji viwili vya Kagulamo na Kyota, Kata ya Kimwani.

Na mradi wa maji Kasharunga mpaka sasa ukarabati umegharimu Tsh. 189 na kazi zilizofanyika ni kulaza bomba lenye urefu wa kilomita 17, kujenga na vituo 24 vya kuchotea maji, ukarabati wa matenki mawili moja likiwa na lita za ujazo 45,000 na la pili likiwa na lita za ujazo 35,000. Kazi inayoendelea kwa sasa ni ujenzi wa tenki la kukusanyia maji lenye lita za ujazo 50,000. Mradi huu unanufaisha vijiji 4 vya Kasharunga, Nkomero, Runazi na Kiguzi vyenye wakazi zaidi ya 15,000.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano, Halmashauri ya Wilaya ya Muleba



 

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa