• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

KAIMU MKURUGENZI MTENDAJI AWASISTIZA WANANCHI KUTOA USHIRIKIANO KUTOKOMEZA VITENDO VYA UKATILI KWA WATOTO

Imewekwa : June 16th, 2022

Katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika ambayo yamefanyika  katika viwanja vya Shule ya Msingi Nshambatapa kata ya Nshamba wilayani Muleba Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Emmanuel Masha amewasistiza wazazi kuhakikisha wanatoa ushirikiano kutokomeza vitendo vya ukatili kwa watoto.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji amesema kuwa endapo matukio ya kiukatili yakifanyika ni vema wananchi wakatoa taarifa haraka ndani ya masaa 24 kuanzia ngazi ya familia, vijiji, kata, ustawi wa jamii na vituo vya polisi ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa wanaofanya vitendo hivyo.

"Hivi vitendo vya kiukatili vinavyotokea sio vya kuvumilia wala kuvifumbia macho inabidi tuwe na mikakati ya kuvikomesha na kuvitokomeza hivyo nawasisitiza wazazi na viongozi wote kuhakikisha vitendo vya ukatili kwa watoto vikitokea hatua kari zichukuliwe ili kutokomeza vitendo hivi" amesema Ndg. Emmanuel Masha.

Aidha, Amewomba wazazi na walezi kuhakikisha kila mtoto mwenye umri wa kwenda shule anaandikishwa na kupelekwa shule na kusisitiza uongozi wa shule za msingi na Sekondari kuhakikisha wanazitumia zahanati na vituo vya afya kupima mimba kwa wanafunzi kila robo mwaka ili kupunguza mimba mashuleni.

Sambamba na hayo ametoa wito kwa jamii taasisi na mashirika kuendelea kutoa huduma za mahitaji muhimu kwa wenye virusi vya UKIMWI pamoja na watoto yatima na kutowanyanyapaa wenye virusi vya UKIMWI.

Katika risala iliyosomwa na Groly Humprey mwanafunzi wa darasa la nne shule ya msingi Nshambatapa kwa niaba ya watoto  wameiomba Serikali kuhakikisha sheria ya kumlinda mtoto inazingatiwa ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua kali kwa wale watakao bainika kufanya vitendo vya ukatili kwa watoto.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika tarehe 16, juni 2022 inasema "Tuimarishe ulinzi kwa Mtoto; Tokomeza ukatili dhidi yake. Jiandae kuhesabiwa ikiwa inasisitiza kuimarishwa kwa ulinzi kwa mtoto kwa kutokomeza ukatili dhidi yake na kuwasihi wananchi wajiandae kuhesabiwa katika zoezi la Sensa ya watu na Makazi ya tarehe 23, Agosti 2022.

Imeandaliwa na kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa