• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

HALMASHAURI YA MULEBA YAJINYAKULIA MAKOMBE 18 MASHINDANO YA UMISSETA NA UMITASHUMITA.

Imewekwa : August 16th, 2024

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera imekuwa ya nne kwenye michezo ya umisseta ngazi ya taifa huku ikijinyakulia jumla ya makombe 18 ngazi ya Mkoa kwenye michezo mbalimbali iliyochezwa mwaka huu katika shule za msingi  na sekondari.

Akipokea makombe hayo mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Mhe. Magongo Justus kwenye kikao cha baraza la Madiwani robo ya nne amesema kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026 halmashauri itatenga bajeti kwa ajili ya kuwawezesha wanafunzi ili kukuza vipaji.

“Kupitia kikao hiki kuanzia mwaka kesho lazima tuandae bajeti ili tukuze vipaji na zaidi tutoe zawadi tuweze kuwatia moyo vijana wetu,walimu wanaowafundisha na muleba iweze kufahamika kwa kazi inazofanya”

Mhe. Magongo amewapongeza walimu wa michezo kutoka shule za msingi na sekondari kwa kushirikiana kwa pamoja kufanikisha ushindi huo ambao umeweza kuitangaza halmashauri.

“nipende kumpongeza afisa utamaduni na walimu wa michezo kwa namna wanavyotuunganisha sisi viongozi kwani kuwa mshindi wanne kitaifa sio jambo dogo hivyo niendelee kuwapongeza na niombe kila mmoja kuunga juhudi za vijana wetu”.

 Kwa upande wake afisa utamaduni na michezo Wilaya ya Muleba Bw. Denis Joseph amesema wameshiriki michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa pete, mpira wa miguu na mpira wa wavu na kuibuka  kuwa mshindi wa jumla kimkoa .

Pia amesema kwa upande wa fani za ndani yaani kwanya wameshika nafasi ya kwanza kimkoa hivyo halmashauri ya Muleba ilipata nafasi ya kuwakilisha mkoa wa kagera katika mashindano ngazi ya Taifa na kuibuka mshindi wa nne.

Aidha Bw. Denis ameongeza kuwa katika mashindano ya shule za msingi wamepata makombe 7 na upande wa Sekondari makombe 11 ambapo kwenye ushindi wa jumla ngazi ya Mkoa Wilaya ya Muleba iliibuka kuwa mshindi wa kwanza kati ya Halmashauri 8.

Nao baadhi ya walimu wa michezo ambao ni Mwl. Imelda Rukatila na Mwl. Abdala Malongo wamesema kuwa ushindi walioupata umetokana na uanzishwaji wa vitalu vya michezo mashuleni pamoja na ushirikiano mkubwa waliopewa na uongozi wa Halmashauri.

                                                       

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 17-06-2025 June 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 07-05-2025 May 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa