• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

HALMASHAURI MUANZISHE VYANZO VIPYA VYA MAPATO-DC KEMILEMBE

Imewekwa : August 13th, 2022

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Muleba, ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo Mhe. Kemilembe Lwota, ameitaka Halmashauri kubuni vyanzo vipya vya Mapato na kuziba mianya ya uvujaji mapato ili kuongeza makisio ya ukusanyaji wa Mapato.

Akizungumza wakati wa Baraza la kumaliza Mwaka wa fedha 2021/2022, Mhe. Kemilembe amewataka Waheshimiwa Madiwani na Wataalam kuanza kubuni vyanzo vipya vya mapato ili kuongeza wigo wa ukusanyaji mapato, huku wakiendelea kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato.

“Nawapongeza sana kwa ukusanyaji mapato, lakini ni wakati sasa muanze kufikiria na kubuni vyanzo vipya vya mapato. Na wakati huohuo mdhibiti upotevu wa mapato kwani Serikali isiyokusanya mapato haiwezi kuendelea,” ameeleza Mhe. Kemilembe.

Sambamba na hayo amezungumzia juu ya masuala ya kuimarisha hali ya ulinzi na usalama katika maeneo yote ya Wilaya, huku akitoa onyo kwa watu wanaovunja amani kuwa Serikali itawachukulia sheria kali na kukemea tukio la wananchi Kijiji cha Nsambya, Kata ya Nyakabango, kuwashambulia Viongozi wa Serikali wakati wakiwa katika majukumu yao na kumjeruhi Mtendaji wa Kijiji kwa kumkata mapanga kichwani na kwenye mikono. Amemuagiza Kamanda wa Polisi wa Wilaya kuwafikisha watu hao mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.

Ameendelea kuhamasisha maandalizi Sensa ya Watu na Makazi inayotarajia kufanyika tarehe 23.08.2022 kuwa elimu iendelee kutolewa kwa wananchi na watu wawe tayari kuhesabiwa siku hiyo kwa maendeleo ya Taifa leti.

Na mwisho amesisitiza maandalizi ya Ujio wa Mwenge wa Uhuru ambapo kwa mwaka 2022 Mkoa wa Kagera ni mwenyeji wa kilele cha mbio hizo za Mwenge Kitaifa.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa