• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DED, AWAHIMIZA MAAFISA ELIMU KATA KUHAKIKISHA WANAZITUMIA KOMPYUTA WALIZOPEWA KWA MATUMIZI SAHIHI YANAYOHITAJIKA

Imewekwa : May 13th, 2022


Katika Baraza la madiwani lililofanyika ndani ya,Ukumbi wa Halmashauri Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Elias Kayandabila pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Magongo Justus  wamekabidhi Kompyuta 42 kwa Maafisa elimu Kata wa wilaya ya Muleba zilizotolewa na Serikali kwa lengo la kuboreha Elimu.

Akizungumza baada ya kukabidhi Kompyuta hizo  Mkurugenzi Mtendaji ametoa wito kwa Maafisa Elimu waliokabidhiwa Kompyuta kuzitumia kompyuta kwa matumizi ya Ofisi na kuwa hawatarajii kuona Komyuta zimeenda kutumika kwa ajili ya matumizi binafsi.

"Niwaombe Komyuta hizi mkazitunze kwa sababu hivi ni vifaa vya Kierektroniki hivyo havihitaji unyevu na maji kwa maana hiyo mkazitunze vizuri ili ziweze kukaa kwa mda mrefu ili ziweze kutunufaisha na kuwanufaisha Watanzania kwa ujumla kwahiyo nawaomba muendelee kuwa makini zaidi katika utunzaji wa Kompyuta hizi" amesema Ndg. Elias Kayandabila.

Lakini pia Mkurugenzi Mtendaji ameeleza kuwa lengo kubwa la Serikali ni kuboresha taarifa kwa maana ya kuwa na takwimu sahihi za ufundishaji na miundombinu yote ambayo inahitajika kwa ajili ya elimu hivyo Kompyuta hizo zimetolewa kwa matumizi ya ofisi ili ziweze kufanya kazi na kurahisisha mawasiliano.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Muleba Mhe. Magongo Justus ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais. Samia Suluhu Hassan kwa kuelewa na kuona uhitaji wa Halmashauri kwa kutoa Kompyuta kwa Maafisa Elimu Kata.

"Hili lililofanywa na Serikali litatusaidia sana kupunguza matumizi ya Karatasi, kuandika kwa mkono na pia zitaweza kusaidia katika utunzaji wa takwimu mbalimbali kwa shule zetu za msingi na Sekondari hivyo niwaombe Maafisa Elimu kuzitunza Kompyuta hizi" amesema Mhe. Magongo Justus

Khalib Issa Mtabazi Afisa Elimu kata Nyakatanga ameeleza kuwa kupitia msaada huo yeye binafsi amefarijika kwa sababu itaweza kumsaidia katika ukusanyaji wa takwimu na pia kuisaidia wilaya ya Muleba kukusanya takwimu ambazo ni sahihi. 

Naye Mwl. Meriness Kaizilege Maruka Afisa elimu Kata ya Mayondwe ameipongeza serikali kwa kurifikilia na kuona umuhimu kwamba sasa wanastahili kupatiwa vifaa vya kompyuta hivyo itaweza kuwasaidia Sana katika masuala ya mtandao na taarifa nyingine mbalimbali ambazo inabidi zifanyike kimtandao.

Sambamba na hayo ameeeleza kuwa changamoto waliyokuwa nayo awali walipokuwa wanapata changamoto ya kompyuta ilikuwa inatakiwa kuomba msaada kwa wenye kompyuta na wakati mwingine iliwalazimu kwenda kwenye Steshenari ili kupata huduma za kimtandao.

Serikali imetoa Kompyuta 42 aina ya (LENOVO) kwa wilaya ya Muleba kwa Maafisa elimu Kata ambapo kila Kompyuta moja inagharimu kiasi cha shilingi Milioni mbili na laki tano 2,500,000/= hivyo Kompyuta zote zinazokadiliwa kugharimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 100/=

Imeandaliwa na kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 17-06-2025 June 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 07-05-2025 May 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa