• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DED, AMEWASIHI WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA KUZINGATIA WANAYOFUNDISWA NA KUITUNZA MIUNDOMBINU YA SHULE.

Imewekwa : January 17th, 2022

Katika ziara yake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Ndg. Elias Kayandabila alipotembelea shule ya Sekondari ya Anna Tibaijuka, shule ya Sekondari Kasharunga na Shule ya Sekondari Shikizi Kasharunga kukagua mwitikio wa wanafunzi wa kadato cha kwanza kuripoti mashuleni amewasihi wanafunzi kuzingatia wanayofundishwa na walimu mashuleni.

Akizungumza alipozitembelea shule hizo Mkurugenzi Mtendaji amewasihi wanafunzi hao kuitunza miundombinu ya madarasa mapya yaliyojegwa kwa ufadhiri wa fedha za IMF ambapo katika ufadhiri huo Muleba ilipatiwa kiasi cha shilingi bilioni 4.6 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 208 vya sekondari na vyumba 26 vya shule za msingi shikizi.

"Fadhira pekee ambayo tunaweza kumlipa mama Samia Suluhu Hassan Rais wetu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ni kufanya vizuri kwenye masomo yetu kwahiyo niwaombe sasa muweke nguvu kwenye masomo" amesema na kuwasisitiza wanafunzi Ndg. Elias Kayandabila.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji  amewasihi wazazi kuisaidia Serikali kuwatambua na kuwabainisha watoto ambao kwa namna moja ama nyingine wanalazimishwa na wazazi wao kwenda  kuolewa alipofika katika shule ya sekondari shikizi ya Kasharunga na kuwakuta wazazi wakiendelea na zoezi la kuwaleta shuleni hapo watoto wao.

Naye Afisa Elimu Sekondari wa wilaya ya Muleba. Mwl. Jared Muhile amewasihi wanafunzi kuvitunza vyumba vya madarasa bila kuvunja vioo kuharibu mbao za kufundishia na hata vigae vilivyotumika kujengea vyumba hivyo vya madarasa.

Kwa upande wa walimu Afisa elimu Sekondari  amewasihi kuanza mala moja kuzitumia wiki sita za maelekezo kwa wanafunzi ili kuwatengenezea mwanya wa kuweza kuyaelewa watakayofundishwa na walimu.

Mwalimu Paulo Mligo Ambaye ni Mkuu wa shule ya Sekondari Anna Tibaijuka ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kutoa fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa mapya ambayo madarasa hayo  yataweza kuwasaidia kuwaondolea uhaba wa vyumba vya madarasa mashuleni na kuhaidi kwamba watavitunza vyumba hivyo vya madarasa ili viweze kuwasaidia na wanafunzi wengine.

Naye mwanafunzi wa kidato cha kwanza shule ya Sekondari Anna Tibaijuka kwa niaba ya wanafunzi wenzake ametoa shukrani na pongezi kwa uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa na kuhaidi kusoma kwa bidii ili kuweza kuzifikia ndoto zao.

Sambamba na hayo na wazazi pia na wao katika nyakati tofauti tofauti wameeeleza kuwa kupitia fedha iliyotolewa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa vyenye viti na meza imewaondolea changamoto ya kuchangia michango mbalimbali mashuleni hivyo kuwasaidia kuepukana na changamoto ya watoto kwenda na viti na meza mashuleni.

Shule ya Sekondari Anna Tibaijuka leo tarehe 17/1/2022 imewapokea jumla ya wanafunzi 51 ambapo idadi ya wanafunzi wanaotakiwa kuripoti shuleni hapo ni wanafunzi 243 na shule ya Sekondari Kasharunga wameripoti wanafunzi 75 na idadi ya wanafunzi wanaotakiwa kuripoti shuleni hapo ni wanafunzi 269.

Imeandaliwa na kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa