• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC NYAMAHANGA ATOA ONYO KWA VIONGOZI WANAOSHIRIKI KATIKA UVUVI HARAMU KUACHA VITENDO HIVYO

Imewekwa : March 28th, 2023

Katika zoezi la uteketezaji wa Nyavu haramu lilifanyika katika Kata ya Nyakabango Kijiji Katembe Mwalo wa Magarini  Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya Mhe. Dr Abel Nyamahanga ametoa onyo kwa viongozi wanaoshiriki katika vitendo vya uvuvi haramu kuacha tabia hiyo.

Akizungumza na wananchi wa Kata hiyo Mkuu wa Wilaya amesema kuwa kama kiongozi yeyote atabainika akijihusisha na uvuvi haramu hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

"Yeyote ambaye ni kiongozi na anataka kulinda heshima yake ya uongozi afuate maadili ya uongozi ukishakuwa kiongozi lazima uuambie moyo wako utulie ufanye kazi za uongozi na uwe na maadili ya uongozi na sio vinginevyo kushiriki kwenye uvuvi haramu kama serikali hatuwezi kunyamaza kimya tutachukua hatua za kisheria" amesema Mhe. Dr Abel Nyamahanga.

Aidha, Katika oparesheni hiyo amemsimamisha kazi ya Uenyekiti  aliyekuwa Mwenyekiti wa BMU Katika Mwalo huo  Ndg. Thobias Masebwe pamoja na mjumbe wake  Ndg. Juma Salumu  kwa tuhuma za  kufanya wizi wa kamba za mitego haramu na kuzirudisha eneo la kuchomea nyavu haramu baada ya kuwa wamebainika.

Kwa upande wake Ndg. Stanslaus Joseph Mwenyekiti wa Kitongoji Kasheza amesema kuwa nyavu haramu zinaharibu na kuua mpaka samaki wachanga kabisa ambao hawafai hata kuvuliwa hivyo ameiomba Serikali kuwezesha upatikanaji wa nyenzo zitakazotumika kupambana na uvuvi haramu.

Naye Charles Isaka Mkazi wa Magarini amesema kuwa kutokana na kushamili kwa vitendo vya uvuvi haramu vimepelekea upatikanaji wa samaki kuwa  adimu tofauti na ilivyokuwa awali jambo ambalo limesababisha hata samaki kupanda bei tofauti na ilivyokuwa awali.

Katika taarifa iliyosomwa na Afisa Uvuvi wa Wilaya ya Muleba Ndg. Wirifred Tibendelana ameeleza kuwa katika doria 28  zilizofanyika kwa kipindi cha miezi mitatu jumla ya kokoro 80, nyavu za timba 217, nyavu ndogo za makila 320, tupatupa 3 zimekamatwa katika doria hiyo na nyavu hizo zote zinakadiliwa kuwa na thamani ya jumla ya kiasi cha Tsh. milioni 97.7.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mahusiano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

 

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa