• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC, NYAMAHANGA AHIMIZA ELIMU KUTOLEWA KWA WANANCHI JUU YA UMUHIMU WA KAMPENI YA POLIO

Imewekwa : September 8th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhe. Dkt Abel Nyamahanga amewasihi wajumbe waliohudhulia katika kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi kwenda kutoa elimu kwa wazazi wa watoto wenye umri chini ya miaka 8 kuhakikisha wanajitokeza ili watoto wao waweze kupata huduma ya chanjo ya polio.

Akizunguza katika kikao hicho  Mkuu wa Wilaya amesema kuwa elimu ikitolewa kwa wazazi na walezi wa watoto wataona umuhimu wa watoto wao kuchanja chanjo ya Polio ambayo itawalinda dhidi ya maambukizi ya virusi vya Polio.

"Tusisite kuwambia  tuwambie wananchi juu ya umuhimu na madhara ya kutochanja watoto chanjo ya polio" amesema Mhe. Dkt Abel Nyamahanga.

Katika Tarifa iliyosomwa na  Mratibu wa Chanjo ya Polio Wilaya ya Muleba Bi. Christina Mlemi ameeleza kuwa ugonjwa wa pllio umelipotiwa katika Manispaa ya Sumbawanga Mkoa wa Rukwa mnamo tarehe 29/06/2023 kwa mtoto wa umri wa muaka mmoja na miezi 11 ambaye vipimo vyake vilipelekwa maabara ma kutoa majibu chanya.

Hivyo, kutokana na mlipuko huo Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na wadau wa tokomeza Polio waliamua kampeni hii ifanyike katika Mikoa sita ambayo inamuingiliano ambayo ni Kagera,Katavi,Kigoma, Rukwa, Mbeya, na Songwe.

Aidha, ameongeza kwa kusema kuwa ugonjwa wa Polio husababishwa na virusi vya polio ambavyo husababisha mtoto kulemaa na huingia mdomoni kwa njia ya kunywa maji au kwa njia ya kula vyakula ambavyo vimechafuliwa na kinyesi, mtoto  asiyepata chanjo ya polio ni hatari katika maisha yake yote na jamii nzima kwa ujumla kwa sababu huambukizwa kutoka kwa mtoto mmoja kwenda kwa mtoto mwingine.

Akizungumzia lengo la Kampeni ya Polio ni kuongeza uelewa kwa wanajamii kuhusu faida za chanjo ya Polio ambapo chanjo ya polio ndio kinga pekee ambayo inaweza kumlinda mtoto dhidi ya ugonjwa huo.

Kampeni hii itaanza rasmi kuanzia tarehe 21-24/09/2023 kwa ajili ya kuwalinda na kuwazuia watoto wote chini ya miaka 8 kuenea kwa virusi vya Polio na kupitia Kampeni hii Halmashauri ya wilaya ya Muleba inalenga kuwachanja jumla ya watoto laki 160,324.

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa