• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC, NGUVILA AHIMIZA WATUMISHI WASAIDIZI WA OFISI KUPEWA KIPAUMBELE KATIKA MASUALA MBALIMBALI

Imewekwa : March 18th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Muleba  Mhe. Toba Nguvila amesisitiza na kuhimiza watumishi wasaidizi wa ofisi kupewa kipaumbele na kuwajali katika masuala mbalimbali katika kikao kilichofanyika ndani ya Ukumbi wa Halmashauri baina ya Mkuu wa wilaya na watumishi wa serikali ili kutatua kero zao.

Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa wilaya amewaomba  wakuu wa Idara kukaa vizuri na watumishi wasaidizi kwani hata wao wanasaidia kwa kiasi kikubwa kufanikisha kazi za kiofisi.

"Ni vizuri mkawa na desturi ya kuwajali hawa watumishi wasaidizi wa ofisi kwa sababu ni watu muhimu msipowajali mtaumia wenyewe siku moja, sitaki nisikie malalamiko kutoka kwa hawa kwahiyo ni vizuri mkawazingatia" amesema Mhe. Toba Nguvila.

Aidha, Mkuu wa wilaya amuagiza mdhibiti mkuu wa ubora wa shule wilaya ya Muleba kuwa anatembelea na kukagua maendeleo ya shule ili kufuatilia maendeleo ya taaaluma katika shule zote za wilaya.

Sambamba na hayo amewaagiza Maafisa Tarafa, Waratibu elimu wa Kata na Watendaji wa Kata kuhakikisha wanawahimiza wazazi kuchangia vyakula mashuleni ili kuwawezesha wanafunzi kufaulu vizuri kupitia uwepo wa huduma ya  chakula cha mchana wawapo mashuleni kwani itawasaidia kusoma na kuelewa wanayofundishwa na walimu wawapo mashuleni.

Lakini pia amewaagiza walimu wa michezo kusimamia vizuri michezo mashuleni ikiwa ni pamoja na michezo ya UMISETA na UMITASHUMITA ili kuweza kuwapata vijana ambao wana uwezo mzuri katika michezo mbalimbali.

Mkuu wa wilaya amesema kuwa ni lazima iwepo mikataba kwa walimu ya kuongeza ufauru kwa wanafunzi  ili waweze kuongeza jitihada katika kufaurisha wanafunzi ili Wilaya ya Muleba iweze kufanya vizuri na kuwa ya kwanza kitaaluma jambo ambalo amesema linawezekana kama hatua hiyo itachukuliwa.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Muleba Ndg. Charles Ntaki amesema kuwa suara la chakula mashuleni kwa wanafunzi ni suara muhimu sana hivyo ni muhimu wazazi kuchangia chakula mashuleni, lakini pia amesema ofisi ya Mkurugenzi walishagiza uanzishwaji wa mashamba mashuleni ya kuzalisha nafaka ili suara la kuwagalamia watoto chakula liweze kuwa jepesi.

Naye Afisa Utumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Muleba Ndg. Christopher Donatus amewaomba watumishi wote kutambua kwamba wao ndio wasadizi wakubwa wa Mkurugenzi na Mkuu wa wilaya katika kusimamia rasilimali zilizopo katika wilaya ya Muleba pamoja na kusimamia watumishi hivyo ni wajibu wao kuwa na nidhamu na maadili ya kiutumishi ikiwa ni pamoja na kuwasimamia hata watumishi wengine waliopo katika ngazi za chini.

Mdhibiti ubora wa shule wilaya ya Muleba Ndg. Josephat Masiko ameomba viongozi wa  ngazi ya shule wasimamie kuandaa mpango wa jumla wa maendeleo ya shule ambao unatekelezwa kila baada ya miaka mitatu unawaoshirikisha viongozi wote wa kijiji ili kuweza kupunguza matatizo ya shule.

Imeandaliwa na Kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa