• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC, MULEBA AWAHIMIZA MADIWANI KUSIMAMIA MIRADI YA SERIKALI

Imewekwa : February 11th, 2022

Katika Baraza la Madiwani lililofanyika ndani ya Ukumbi wa Halmashauri Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila amewaomba waheshimiwa madiwani kusimamia miradi yote ya serikali inayotekelezwa katika kata zao.

Akizungumza katika Balaza hilo Mkuu wa wilaya amewasihi madiwani kuhakikisha miradi yote ya Halmashauri, TARURA, TANESCO, TANROAD kuhakikisha wanaisimamia kwa sababu inawagusa wapiga kura wao.

"Niwaombe sana miradi yote simamia kila wakati tenga mda wako wa kupitia na kama kuna shida ita wataalamu wa Halmashauri waje kufanya ufafanuzi kama kukiwa na shida katika mradi wowote ita wataalamu wanaohusika na mradi huo" ameeleza Mhe Toba Nguvila.

Kwa upande wake Mhandisi wa Ujenzi Eng. Charles Solo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ameeleza kuwa mpango wa Serikali ni kuanzisha anwani za makazi ambao utakuwa ni mfumo unaotambulisha mahali ambapo mtu anaishi, mahali ilipo biashara yake, au ofisi anayofanyia kazi kwa kufuata jina la barabara na mtaa, namba ya nyumba au jengo pamoja na postikodi.

Amewaeleza Waheshimiwa madiwani kuwa dhamira ya uanzishwaji wa Anwani za makazi ni kuhakikisha utekelezaji wa anwani za makazi kabla ama ifikapo mwezi Mei, 2022 kwa kuhakikisha kila nyumba jengo lina anwani ya makazi.

Mkuu wa wilaya ameomba na kusisitiza kuhakikisha kila mtu anajipanga kwa nafasi yake kuhakikisha anashiriki vizuri katika zoezi la uanzishwaji wa anwani za makazi kuanzia uratibu utekelezaji na usimamizi mpaka kufikia mwisho wa zoezi zima.

"Ni lazma tushiriki kwa mikono yetu miwili kuhakikisha zoezi hili la anwani na makazi linafanikiwa vizuri kuliko hata Halmashauri nyingine zote" amesema Mhe. Toba Nguvila.

Sambamba na hayo amewasihi Waheshimiwa madiwani kuhakikisha wanasimamia katika kata zao  ili kuondosha uvuvi haramu kwa kuwaeleza kuwa uvuvi haramu ukiendelea utadhoofisha mapato ya Halmashauri, ajira zitapotea na samaki watapungua hivyo amewaomba waheshimiwa madiwani kuhakikisha wanasimamia hilo.

Lakini pia ametoa onyo na kusisitiza kamati ya Usalama ya wilaya ya Muleba kuhakikisha wanafuatilia na kubaini mtu aliyehusika na suara la kuvujisha nyaraka ya Kiserikali ya Halmashauri kuhakikisha hatua kali zinachukuliwa juu yake.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Magongo Justus amesema kuwa ameshamuagiza Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili kuanza kushughulikia suara la uvujishaji wa nyaraka ya Halmashauri ili kama ni kwa madiwani hatua za kimadili ziweze kuchukuliwa.

Imeandaliwa na Kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 17-06-2025 June 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 07-05-2025 May 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa