• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC, AZINDUA RASMI SOKO LA SAMAKI NA DAGAA KATEMBE

Imewekwa : August 22nd, 2021

Mkuu wa wilaya ya Muleba Mh. Toba Nguvila amezindua rasmi soko la biashara ya samaki na dagaa katika Tarafa ya Kimwani kata Nyakabango kijiji Katembe  eneo la Magarini.

Mwalo wa Katembe -Magarini, uliopo kijiji Katembe kata Nyakabango wilaya ya Muleba Mkoa wa Kagera ni miongoni mwa mialo inayotegemea sana jamii hususani ya wavuvi kwa biashara ya mazao ya samaki kutoka katika visiwa vya mazinga na Ikuza.

Akifungua soko la samaki Mkuu wa wilaya ya Muleba, Mh.Toba Nguvila amewataka wavuvi kuachana na uvuvi haramu ili kuweza kulinda raslimali za ziwa Victoria kwani kwa sasa wilaya imeweka mpango madhubuti wakulinda na kuhifadhi mazalia ya zao la samaki na kuhakikisha uvuvi haramu unakomeshwa.

"Tumefungua Soko hili kwa sababu ya ajira kwa watu wa Muleba hasa wa eneo hili la Nyakabango kwa maana ya kwamba mama lishe watafanya biashara ya kuuza chakula kwa wageni watakao kuja kununua mazao ya samaki na vijana wetu wa Nyakabango watapata ajira ya kupakia na kushusha samaki kwa sababu kuna jengo tayari la soko la dagaa na samaki wakavu" ameeleza Mh. Toba Nguvila.

Aidha amewataka wadau wote wa uvuvi kuchangamkia fursa ya soko hilo kwani Uongozi wa wilaya umeweka utaratibi mzuri wa kuhakikisha biashara hiyo inawanufaisha watu wote watakao husika.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Muleba Bw. Elias Kayandambila amesema kufunguliwa kwa soko hilo litasaidia kuwarahisishia wavuvi na wafanya biashara wamaotoka visiwani kuja kuuza mazao yao ya samaki katika Mwalo wa Katembe Magarini sambamba na kuongeza mapato kwa Halmashauri kwani zaidi ya shilingi billioni tatu za mapato yanakusanywa na Halmashauri kutokana na mapato ya uvuvi.

Pamoja na kuzindua soko hilo Mh. Toba Nguvila ameongoza zoezi la uteketezaji wa zana haramu za uvuvi zilizokamatwa maeneo mbalimbali wilayani Muleba wakati zoezi la operesheni ya kuondoa uvuvi haramu linaendelea.

Zana zilizoteketezwa ni pamoja na kokolo za kuvuta 210, timba vipande 31, Nyavu za makila (nchi 6) 51, kamba urefu wa mita 3500 na katuli 20, zana hizi haramu zinathamani ya zaidi ya shilingi milioni 197.

Kwa upande wao baadhi ya wavuvi na wafanyabiashara wa samaki na dagaa wameshukuru kwa kitendo cha kufunguliwa kwa soko hilo kutokana na hapo awali walikuwa wanasafirisha kupitia kwenye soko la dagaa la wilaya jirani ya chato na walikuwa wanatozwa ghalama kubwa ya kusafirisha na tozo.


Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa