• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC ATOA MDA WA SIKU SABA KWA WANAFUNZI WALIOCHELEWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA

Imewekwa : March 3rd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhe. Dr Abel Nyamahanga amewaagiza wazazi kuwapeleka watoto waliochelewa kuanza masomo ya kidato cha kwanza kuanza masomo kabla ya tarehe 10/03/2023.

Akizungumza na wazazi pamoja na wanafunzi Mkuu wa Wilaya amewasihi wazazi kutokitumia kigezo cha umasikini kama sababu ya kutowapeleka shuleni wanafunzi.

Wazazi tunatumia kigezo cha umasikini tunakwepa kutoa mahitaji kwa watoto na kuwashawishi watoto wasiende shule sasa tarehe 10 ndio mwisho wa huruma hii inapofika terehe 13 watoto wote wawe shuleni.

Aidha, amewaeleza wazazi kuwa hawawezi kukikomboa kizazi cha masikini bila kuwapeleka watoto shule hivyo ni vyema wakawapeleka watoto shule ambao wakipata elimu wataweza kuzinufaisha familia zao na kuondoa hali duni kwenye familia wanapotokea.

Lakini pia amewasihi wazazi kutowakatisha tamaa watoto wao kuikataa shule kwa kisingizio cha mazingira magumu wanayotokea ni vema wakawaelezea juu ya umuhimu wa elimu ili wawe na moyo wa kuipenda shule.

Naye Ndg. Philibert George Mwenyekiti wa Kitongoji cha Nyakabango ameshauri uwepo wa ufuatiliaji wa mahudhulio ya wanafunzi ambao tayari wamesharipoti mashuleni na ambao wataanza kuripoti mashuleni ili kuweza kukomesha changamoto ya wanafunzi kuhudhulia kwa mda na baadae kuacha shule.

Moses Simoni mwanafunzi aliyechelewa kuanza masomo ya kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Nyakabango ameeleza kuwa changamoto iliyomkwamisha kuanza masomo kwa wakati ni kutokana na hali ngumu ya kimaisha na kuiomba Serikali kutoa msaada kwa wenye maisha magumu ili na wao waweze kupata elimu.

Naye Vedastus Laulent ambaye pia ni mwanafunzi aliyechelewa kuanza masomo ya kidato cha kwanza ameonyesha utayari wa kuanza masomo hayo kama akisaidiwa kwa mahitaji anayopungukiwa na ameshauri kwa wanafunzi wenzake ambao na wao hawajaanza shule wasikae nyumbani waanze shule ili waweze kunufaika na elimu.

Mkuu wa Wilaya amefanya ziara hiyo katika shule ya Sekondari Nyakabango, Shule ya Sekondari Dr Ishengoma Kikoyo, Shule ya Sekondari Kimwani na Shule ya Sekondari Kyebitembe.

Imetolewa na:

kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.


Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 17-06-2025 June 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MULEBA 07-05-2025 May 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa