• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC, AMEWAAGIZA VIONGOZI WA KATA YA RUTOLO KUTOWAINGIZA WATU KINYEMELA KWENYE MAENEO YAO ILI KULINDA USALAMA WA ENEO HILO.

Imewekwa : January 13th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila katika ziara yake alipovitembelea vijiji vya kata ya Rutolo wilayani Muleba amewahimiza viongozi wa Tarafa,  Kata, Vijiji na Vitongoji wa Rutolo kuhakikisha wanasimamia ili kuzuia watu kuingia kinyume na utaratibu katika eneo hilo. 

Akizungumza katiza ziara hiyo alipovitembelea vijiji vinne vya kata ya Rutolo ambavyo ni Byengeregere, Rutolo, Kyobuheke na Nshabya amewasihi wananchi kuhakikisha hawaruhusu watu kuingia kinyume na utaratibu katika eneo hilo bila idhini yake Mkuu wa wilaya ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kuruhusu mtu aingie au asiingie ambapo amewaeleza kuwa mwenye idhini ya kuingiza watu na hata Mifugo ni yeye Mkuu wa wilaya na Kamati yake ya usalama. 

"Niwaagize viongozi wote wa tarafa wa kata wa vijiji wa vitongoji kwenye hili msimamie mseme sasa basi hajuhitaji kuingiza ingiza watu kinyemela ninyi mliopo mnatosha kama watu wanaingia wafuate utaratibu" ameendelea kusema.

"Ni lazima ifike hatua mkae vizuri mfanye shughuli zenu za kiunchumi, kijamii, na za kisiasa bila kuwa na mitafaruko mitafaruko haijengi utengamao kwenye eneo na ndio maana tuko hapa tumeamua tumedhamilia sasa hizi hofu hofu mda wote ziishe sasa" amesema Mhe Toba Nguvila.

Aidha, amewaeleza wananchi wa Rutolo kuwa wameshaka na NARCO pamoja na kamati ya usalama na waziri wa mifugo na uvuvi ambapo walikubaliana namna ya kuwapanga katika maeneo mazuri ambayo wanaweza wakalima na kuzalisha ili kuepuka njaa ambapo amewaeleza kuwa itakuja kamati ambayo itakuwa na wataalamu wote wa kubainisha maeneo bora ya wao kulima.

"Kwa wale ambao tutawatoa kutoka maeneo ya mbali   ambao wataathirika kuletwa kwenye haya maeneo   watatengewa hekali sita sita kila familia ili wajenge na wapate sehemu ya kulima jambo la msingi viongozi wote wa kata wa vijiji wa vitongoji mshiriki kikamilifu kwenye zoezi ili msaidie kurahisisha kazi ya kamati kamati itakuja hapa ninyi muikumbatie muwe marafiki ili zoezi liwe rahisi liishe haraka" amesema Mhe. Toba Nguvila.

Lakini pia amewaomba na kuwasisitiza wananchi wa eneo hilo kuhakikisha wanakuwa walinzi wakubwa wa vitalu kwa sababu vitalu vinaenda kupunguzwa kwa ajili yao ambapo amewambia kuwa wakishapangwa vizuri wawe marafiki na wenye vitalu ambao watawasaidia ili hata wakati wanajenga shule wawasaidie kuchangia saruji na mabati.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Muleba Kaskazini Mhe. Charles Mwijage amewaeleza kuwa wakiwa karibu kutoka maeneo ya mbali huduma za kijamii zitaweza kuwafikia kila mwananchi ikiwa ni pamoja na umeme na maji ambapo amewaeleza kuwa wakikaka kwa kutawanyika itakuwa ni vigumu hata kuwepo kwa urahisi kwa walioko mbali kupata huduma za umeme, maji pamoja na shule.

Mwisho, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Muleba Mhe. Athuman Kahara amewaeleza wananchi wa eneo hilo kuwa kwa walio mbali wanakwenda kupangiwa maeneo mazuri ya kilimo ambayo yatawasaidia kulima na kuzalisha miaka yote pamoja na vizazi vyao vyote.

"Unapoona unakwenda kumiliki kile ambacho ni halali hiyo ndo faida mtakayoipata tangu leo sisi kama chama pamoja na serikali wale wote watakaotengewa maeneo ya hekali sita sita  ni wale ambao watakuwa kwenye maeneo tayari adui watakuwa ni wale watakaukuja kupangiwa wakakutwa walikuwa hawana makazi kabla ya kugawiwa maeneo" amesema Mhe. Athuman Kahara.

Imeandaliwa na kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa