• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC, AHIMIZA WANAWAKE KUPEWA KIPAUMBELE KATIKA FURSA MBALIMBALI ZA KIMAENDELEO ILI KUWAINUA KIUNCHUMI

Imewekwa : March 9th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila  katika maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika katika kijiji cha Rulanda Kata ya Rulanda wilayani Muleba amehimiza wanawake kupewa fursa mbalimbali za kimaendeleo ili kuondoa ongezeko la wimbi kubwa la wanawake wanaoishi katika hali ya umaskini.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Mkuu wa wilaya ya Muleba amesema kuwa wanawake wakipewa fursa mbalimbali itawasaidia kupata ajira, kuongezeka  kwa vipato katika familia na kuondoa wimbi kubwa la jamii inayoishi katika umaskini.

"Ni lazima sisi kama Serikali tuone namna ya kuwasaidia wanawake na ni jukumu letu kuhakikisha wanawake wote bila kujali hali zao wanapata haki zao zote za msingi zinazohitajika kwa ajili ya kuleta maendeleo chanya katika uchumi wa viwanda"

Aidha,  Amewaomba na kuwahamasisha wanawake wa wilaya ya Muleba kuanzisha vikundi na kukopa fedha kutoka Halmashauri kwa ajili ya kuanzisha biashara na miradi mbalimbali itakayosaidia kuinua hali zao kiuchumi.

Lakini pia amewaomba wananchi kujitokeza katika zoezi la sensa ya watu na makazi litakalofanyika kitaifa mwezi wa nane mwaka huu ili serikali iweze kujua idadi ya watu wote katika nchi kwa umri wao jinsia mahali wanapoishi na hali ya elimu hali ya ajila na hali ya vizazi na vifo pamoja na hali ya makazi ili kupitia takwimu hizo serikali iweze kuainisha mahitaji ya msingi ya wannchi na taifa kwa ujumla.

Sambamba na hayo amewaeleza wanawake kuwa ni watu muhimu kwenye familia na jamii kwa ujumla hivyo wanatakiwa kusimama kwenye nafasi yao kuisaidia jamii na Tanzania kwa ujumla kwasababu wao ndio nguzo ya kweli walezi na ni kioo kwenye jamii.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Muleba Mhe. Magongo Justus amewaomba wanawake wote kupitia siku hiyo ya wanawake iwahamasishe kuwa walimu wa kweli walinzi wa kweli na wawe pia wazazi wa kweli pamoja na kuifanya dunia iwe nimahara salama na bora pa kuishi.

Katika risala yao iliyosomwa na Bi. Asuma Abdalah  wameomba kuwawezesha wanawake kufikia Tanzania ya viwanda ni lazima kuwe na uwekezaji katika sekta ya kilimo hivyo wameomba kusaidiwa  kupata pembejeo huduma za ugani kutafta masoko na juhudi hizo ziende sambamba na upatikanaji wa teknolojia rahisi ya uzalishaji mali katika kukamilisha mzunguko wa myororo wa thamani ili kuchangia ipasavyo katika Tanzania ya viwanda.

Lakini pia wameomba kutengewa eneo ambalo lutakuwa eneo la uzalishaji hasa katika nyanja ya viwanda pamoja  na kuwa na miundombinu ya umeme maji barabara na kadhalika

Kauli Mbiu ya Mwaka huu inasema kuwa "Kizazi cha haki na usawakwa maendeleo endelevu tujitokeze kuhesabiwa" kauli mbiu inasisitiza umuhimu wa usawa wa kijinsia katika kuleta maendeleo ya kweli na yanayonufaisha makundi yote katika jamii hapa nchini pamoja na kuwakumbusha wananchi kushiriki katika zoezi la sensa ya idadi ya watu na makazi.

Imeandaliwa na Kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa