• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC AHIMIZA WANANCHI KULINDA NA KUTUNZA MIUNDOMBINU YA MAJI.

Imewekwa : March 22nd, 2023

Katika Maadhimisho ya Wiki ya Maji Duniani iliyofanyika Kata ya Kamachumu Kijiji cha Bulamula Wilaya ya Muleba Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhe. Dr Abel Nyamahanga amewahimiza wananchi kulinda na kutunza miundombinu ya maji ili iweze kudumu kwa mda mrefu.

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi katika tenki la Mradi wa Maji wa Bulamula amewaeleza wananchi kuwa ni wajibu wao kulinda miundombinu ya maji dhidi ya uhalifu ambao unaweza kujitokeza.

"Wapo watu wengine sehemu linakopita bomba la maji wanajenga nyumba huu sio utaratibu na wala sio usitaarabu tusifanye hivyo pahala penye bomba la maji tujenge pembeni hivyo niwasihi muepuke kujenga na kulima kwenye miundombinu ya maji ili miundombinu hii iendelee kutuhudumia kwa mda mrefu " amesema Mhe. Dr Abel Nyamahanga

Aidha, Mkuu wa Wilaya amewahimiza wananchi wa Kijiji cha Bulamula kuwa kukamilika kwa mradi huo kulete tija katika kuchangia mabadiliko chanya ya uchumi endelevu ambapo amewasihi kuwa maji yatumike na yalete thamani katika kukuza shughuli za kiuchumi.

Lakini pia amewahimiza wananchi kupanda miti katika vyanzo vya maji ili kusaidia kutunza maji na kuchangia upatikanaji wa maji katika vyanzo hivyo.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa RUWASA Mkoa wa Kagera  Mhandisi Patrice Jerome ameeleza kuwa kwa kipindi cha Miaka Miwili ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan hali ya huduma za maji imeendelea kuimalika wilayani Muleba ambapo zaidi ya asilimia 80 ya wananchi wa Wilaya ya Muleba wanapata huduma za maji.

Pamoja na hayo ameongeza kwa kusema kuwa zaidi ya miradi 11 inatekelezwa katika Wilaya ya Muleba ambapo kati ya miradi hiyo kuna miradi imekamilika na imeshaanza kutoa huduma na kuna miradi inaendelea kutekerezwa na jumla ya vijiji 27 vinaenda kunufaika na miradi hiyo ya maji  inayotekelezwa kwa gharama za kiasi cha Tsh. Bilion 11 na zaidi ya wanachi elfu 75178 watanufaika na miradi hiyo.

Katika Maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya ametembelea na kukagua chanzo cha Mradi wa Maji wa Ilemera unaotekelezwa kwa kiasi cha Tsh. Milioni 599, tenki la  Mradi wa Maji Kagoma unaotekelezwa kwa kiasi cha Tsh. Milioni 680 pamoja na kuweka jiwe la msingi katika  Mradi wa Maji Bulamula unaotekelezwa kwa kiasi cha Tsh. Milioni 681.

Imetolewa na:

Kitengp cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa