• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC , AFANYA UZINDUZI WA MELI YA JUBILEE HOPE KUTOA HUDUMA ZA AFYA KATIKA VISIWA VYA WILAYA YA MULEBA

Imewekwa : January 21st, 2022

Mkuu wa wilaya ya Muleba  Mhe. Toba Nguvila amezindua rasmi shughuli za utoaji wa huduma za afya unaofanywa na Meli ya Jubilee Hope inayomilikiwa na Kanisa la African Inland Church Tanzania katika kisiwa cha Chakazimbwe Kata ya Ikuza wilayani Muleba.

Akizungumza baada ya uzinduzi wa Meli hiyo Mkuu wa wilaya ya Muleba amewaomba wananchi wa kisiwa cha  Chakazimbwe kuendelea Ku to a ushirikiano mkubwa kwa kanisa la African Inland Church Tanzania na kuwasihi kuwatangazia wenzao kuja kupata huduma za afya katika meli hiyo ili waweze kupona maradhi mbalimbali.

"Ndugu zangu changamkeni kupata tiba katika Meli hii Mungu amewapendelea ninyi ukiwa unaumwa, unakohoa, unajisikia tumbo kuuma au ukajisikia homa nenda kapime uwe na bima uwe huna bima unakwenda unapata huduma bure bila malipo"  amesema Mhe Toba Nguvila.

Aidha, Mhe Mkuu wa wilaya amewaomba Madiwani, Watendaji na Wenyekiti wa vijiji na Vitongoji wa kuhakikisha wanatoa ushirikiano wa kutosha kuilinda huduma hiyo lakini pia amewaagiza wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama kuweka vyombo vinavyoonekana na visivyoonekana kuhakikisha kuhakikisha kwamba hakuna hujuma yeyote wala mtu yeyote wa kuhujumu huduma  ya afya inayotolewa na Meli ya Jubilee Hope pamoja na kuhakikisha wanaweka ulinzi kwa wataalamu wanaotoa huduma katika Meli Hiyo.

"Msipoilinda hii Meli ninyi maana yake mnajinyima wenyewe kupata huduma bora ya afya kupitia Meli hii na wataalamu wake kwahiyo ulinzi wa hawa uwe kwenu" amewasihi wananchi Mhe. Toba Nguvila.

Lakini pia Mhe. Mkuu wa wilaya amewaomba watoa huduma katika Meli hiyo kuendelea kutoa huduma nzuri na bora chini ya usimamizi wa Kanisa la African Inland Church kwa ushirikiano wa Serikali ya wilaya ya Muleba na kuwahaidi  kuwa kama serikali watahakikisha kuwa watakuwa salama mda wote ili waendelee kutoa huduma bora kwa wananchi wa Muleba.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Ndg. Elias Kayandabila amewaeleza wananchi kuwa kwa sasa zipo jitihada ambazo zinafanywa na wilaya kuhakikisha wanasuruhisha tatizo la huduma kwenye sekta za afya ambapo amewaeleza kuwa kwa mwaka wa fedha 2022- 2023 tayari Halmashauri imeanza ujenzi wa kituo cha afya kwenye kata ya Bumbile kwa kutumia mapato ya ndani ya Halmashauri.

Mkurugenzi Mtendaji pia amewaeleza  kuwa tayari zimeshapelekwa pale Milioni 350 ili kujenga kituo cha afya na kuwaeleza kuwa Kabla ya mwaka kuisha zitapelekwa milioni 150 kwa ajili ya kituo hicho cha afya.

Sambamba na hayo Mkurugenzi Mtendaji ametoa shukrani kwa kanisa la African Inland Church pamoja na taasisi ya Vine Trust iliyopo Wingereza pamoja na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (Geita Gold Mining GGM) na Serikali hasa Mhe Rais kwa kuweza kukubali kuletwa kwa chombo cha Meli ya Jubilee kuwahudumia wananchi wa Muleba.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Muleba Mhe. Justus Magongo ametoa Shukrani kwa Meli kanisa la African Inland Church kwa huduma ya afya wanayoitoa kwa watu wa visiwani lakini pia kwa niaba ya wananchi wa Muleba Amemthibitishia makamu baba  askofu wa kanisa hilo  Mchungaji Obed Nkulukulu  kwamba Muleba wako Tayari kuendelea kushirikiana kwa namna yeyote na shughuli inayoendelea katika Meli ya Mv Jubilee Hope kwa kuwaeleza kuwa kama kutakuwa na hitaji la msaada wowote Kutoka Halmashauri ya Muleba kuwa wako tayari kutekeleza.

Naye Katibu wa Siasa na Uenezi wa  Chama cha Mapinduzi  Ndg. Theonest Thadeo  amewapongeza sana watumishi wa Meli ya Mv Jubilee kwa kujitoa kwa dhati kutumikia eneo la visiwani pamoja na kutoa shukrani za kipekee kwa  Mgodi wa Geita (GGM) na Shirika Vine Trust kwa kuchukua jukumu la kutoa huduma za  afya kwa kuliona na Kutoa kipaumbele kwa ajili ya afya za wananchi wa Visiwani.

Imeandaliwa na Kutolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa