• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC, AAGIZA MAFUNDI KUFANYA KAZI BILA UZEMBE ILI KUMALIZA HARAKA UPANUZI WA MAJENGO KITUO CHA AFYA KAMACHUMU

Imewekwa : February 16th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila katika ziara ya Ukaguzi wa Maendeleo ya ujenzi katika Kituo cha Afya Kamachumu amewahimiza Mafundi kuhakikisha wanafanya kazi bila uzembe ili kuweza kumaliza haraka upanuzi wa  majengo katika kituo hicho cha afya ili kiweze kuendele kutoa huduma za afya kwa wananchi.

Akizungumza katika ziara hiyo amewasihi mafundi wakuu kuhakikisha kila jengo linakuwa na mafundi wasiopungua nane na wasaidizi nane pamoja na kuwahimiza Watendaji wa Kata, Afisa Tarafa na Kamati ya ujenzi kuhakikisha kila kitu kinakuwepo ili kuweza kuimarisha kazi kwa mafundi.

"Tukichelewa kuwa na mawe, kuwa na tofari kuwa na vitu vyote vinavyotokea pembezoni mwa barabara kuu tutakwama kwenye ujenzi kwahiyo mawe mchanga na tofari vyote viwe eneo husika ili mafundi wanavyoanza kujenga kusiwe na sababu yeyote inayopelekea kuchelewesha ujenzi"

Sambamba na hayo Mkuu wa wilaya ametoa pongezi kwa kuona ujenzi umeenza tangu fedha zimeingizwa kwenye akaunti terehe 13 ikiwa  ni siku ya pili tangu fedha hizo kuingizwa kwenye akaunti  hivyo amempongeza Mhe. Diwani na wasaidizi wake kwa kuiona  kazi kwa sababu tayari wameshaweka vionwa vitakavyotumika katika ujenzi wa Kituo hicho cha afya.

Lakini pia amemuagiza Mtendaji wa Kata na Kamati ya ujenzi kuhakikisha kila siku ifikapo saa 12 wanatoa taarifa ya maeendeleo ya kazi kwa siku wamefikia hatua gani ili kuona kama kuna uzembe wowote unaoendelea achukue hatua haraka.

Kwa upande wake Diwani wa Kata hiyo Mhe. Leodigard Chonde ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 250 kwa ajili upanuzi wa kituo hicho cha afya na kumhakikishia Mkuu wa wilaya kuwa akiona jambo lolote linaleta shida katika ujenzi wa Kituo cha afya atatoa taarifa na kuhaidi kusimamia usiku na mchana ujenzi huo.

Naye Mganga Mkuu wa Kituo hicho cha Afya Kamachumu Dr Lightness Charles  ameleza kuwa kituo hicho kilikuwa kinapungukiwa na majengo matatu ambalo ni jengo la upasuaji jengo la mama na mama na mtoto na jengo la maabara ya kisasa.

Imetolewa na Kuandaliwa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wilaya ya Muleba

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa