• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA MAPENDEKEZO YA MPANGO WA BAJETI KIASI CHA TSHS BIL.79 KWA MWAKA WA FEDHA 2024-2025.

Imewekwa : February 15th, 2024

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Muleba linaloongozwa na Mhe.Magongo Justus Mwenyekiti wa Halmashauri na Diwani wa Kata ya Muhutwe leo tarehe 14 Februari, 2024 limehitimisha kujadili mapendekezo ya mpango wa bajeti wa Halmashauri kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2024-2025 ambapo limeidhinisha na kupitisha rasimu ya Mpango wa bajeti ya fedha kiasi cha Tshs Bil.79,982,847,750.

Akiwasilisha Mpango wa bajeti Mkuu wa Divisheni ya Mipango na Uratibu wa Halmashauri Ndug.Evart Kagaruki ameeleza kuwa katika kuandaa mpango huu wa bajeti Vipaombele mbali mbali vilizingatiwa ikiwa ni pamoja na  kulipa mishahara ya watumishi,kuendesha vikao vya kisheria,kutoa ruzuku ya uendeshaji wa Shule za Msingi na Sekondari, kuimarisha Miundombinu iliyopo katika maeneo ya kutolea huduma za kijamii na kiuchumi,ukamilishaji wa Miradi viporo,ulipaji wa Madeni ya wakandarasi na watoa huduma wanaoidai Halmashauri,kuendesha mitihani ya ndani na kitaifa(Shule za Msingi na Sekondari),uboreshaji wa huduma za Afya kwa kununua madawa na vifaa tiba na kutoa elimu ya afya na usafi wa mazingira pamoja na kutekeleza miradi yenye lengo la kuongeza mapato ya Halmashauri kama vile ujenzi wa Jengo la Soko kuu la kariakoo.

Aidha,baraza la Madiwani kwa robo hii ya pili pia limepitisha rasimu ya Mpango wa bajeti ya wakala wa Barabara vijijini na mijini (TARURA) kiasi Cha Tshs Bil.4,300,923,478.

Akiwasilisha mpango wa bajeti Kaimu Meneja Mkuu wa TARURA Mhandisi Dativa K.Telesphory amesema kuwa kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2024-2025 Halmashauri ya Wilaya ya Muleba imeidhinishiwa kiasi Cha Tshs Bil.4,300,923,478.26 kwa ajili ya matengenezo ya barabara kwa kupitia vyanzo vitatu ambavyo ni kutoka mfuko wa Barabara kiasi cha Tshs Bil.1,300,923,478 Shilingi Bil.1,000,000,000 kutoka hazina(Jimbo) na kiasi Cha Tshs 2,000,000,000 kutoka hazina kama tozo ya mafuta.

Imeandaliwa na kutolewa na;

Eusebius J. Kiluwa

KAIMU MKUU KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

 

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa