• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

WANANCHI WILAYANI MULEBA WAHIMIZWA KUCHANJA MBWA WAO ILI KUWEZA KUWAKINGA DHIDI YA MAAMBUKIZI YA KICHAA CHA MBWA

Imewekwa : September 28th, 2022

Katika maadhimisho ya Siku ya Ugonjwa wa kichaa cha Mbwa Duniani yaliyofanyika Kiwilaya katika Uwanja wa Zimbihile Wilayani Muleba  wananchi wameendelea kuhimizwa kuchanja mbwa wao kila baada ya mwaka ili kuwaepushia tatizo la kupata ugonjwa wa kichaa cha mbwa.

Akizungumza baada ya kutoa chanjo kwa baadhi ya Mbwa walioletwa na wananchi ili waweze kupatiwa chanjo hiyo Dr. Emmanuel Kaijage daktari wa mifugo wa Wilaya ya Muleba amewaelezea wananchi kuwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa ni ugonjwa ambao ni hatari sana ambao unaweza kuambukizwa kwa mbwa na huyo mbwa akamuambukiza mwanadamu kwa kumng'ata jambo ambalo linaweza kuhatarisha maisha ya mwanadamu.

"Ugonjwa wa kichaa cha mbwa hauna tiba na mnyama akishadhibitika amepata virusi hivi au binadamu akipata virusi vya kichaa cha mbwa anakuwa hawezi kupona kwahiyo ushauri tunaoutoa kwa wananchi ambao wana mbwa ni kuhakikisha mbwa wao wanapata chanjo ili mbwa akijakung'atwa na mbwa mwenye kichaa amkute huyo mbwa tayari ana kinga asiweze kupata ugonjwa" amesema Dr Kaijage.

Aidha Dr. Kaijage ameongeza kwa kusema kuwa ili kumtambua mbwa mwenye kichaa ni pale ambapo mwananchi ambaye anafuga mbwa ataona mbwa wake anatiririsha mate kutoka mdomoni pamoja kuwa na tabia ya kung'ata kitu chochote anachokiona hivyo mwananchi akiona mbwa wake anadalili hizo ni vema akachukua tahadhari.

Naye Afisa afya na Mazingira wa Wilaya ya Muleba Ndg. Johanes Francis Mutoka amesema kuwa mbwa anapokuwa amepatiwa chanjo hata aking'atwa na mbwa ambaye tayari ana virusi vya kichaa cha mbwa virusi hivo vitaweza kuangamizwa kwa sababu mbwa tayari atakuwa na kinga ya chanjo dhidi ya virusi hivyo.

Kwa upande wake Oliva Angelo mkazi wa Kata ya Muleba ameshauri kuwa ni vema wananchi wakawa wanawapeleka mbwa wao kupatiwa chanjo hata kwenye vituo vya afya ili kuweza kuwaepusha mbwa wao kupata maradhi ya kichaa cha mbwa.

Vedasto Kaigi mkazi wa Kata ya Muleba ameeleza kuwa mbwa akichanjwa inasaidia kuishi kwa amani pamoja na wananchi wengine kwani mbwa akipata ukichaa kama hajachanjwa anaweza kumjeruhi mwanadamu na kumuambukiza ugonjwa wa ukichaa jambo ambalo linaweza kuleta athari katika jamii.

Katika maadhimisho hayo jumla ya mbwa 224 na paka 31 wamepatiwa chanjo ya kichaa cha mbwa

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa