• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

RC KAGERA AWAHIMIZA WANANCHI KUTOA USHIRIKIANO KUPAMBANA NA UVUVI HARAMU

Imewekwa : July 11th, 2022

Katika hafla ya kukabidhi boti kwa ajili ya doria za kudhibiti uvuvi haramu, iliyotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Charles Mbuge amewahimiza wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kupiga vita uvuvi haramu katika ziwa Victoria.

Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyikia katika soko la Magalini lililopo kijiji Katembe, Kata ya Nyakabango, amewahimiza wananchi kuhakikisha kila mmoja anakuwa mlinzi wa mwenzake wa maliasili zilizomo ziwani ili kuweza kuzuia vitendo vya uvuvi haramu unaofafanyika katika ziwa Victoria.

"Naomba mkawambie na wananchi ambao hawakufika hapa wawe wazalendo kwa maliasili zetu tukijiingiza katika vitendo vya uvuvi haramu hatutapata samaki kwa miaka ijayo wala watoto wetu hawataona samaki hao na pia hatutakuwa na lishe bora kwenye miili yetu samaki ni lishe kwa afya zetu" ameeleza Meja Jenerali Mbuge

Aidha, amesema kuwa wale wote watakaokamatwa wakishiriki kufanya uvuvi haramu sheria itachukua mkondo wake na kuelekeza mamlaka zisiwasamehe, taratibu zote zifuatwe bila kumuonea aibu mvuvi haramu yeyote.

Sambamba na hayo ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kupitia wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kutambua umuhimu wa kuwa na boti ya kufanya doria kudhibiti uvuvi haramu ili hata vizazi vijavyo viweze kunufaika na mazao ya samaki.

Taarifa iliyosomwa na Masanja Lukasi Kadashi Afisa Mfawidhi wa Uvuvi, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeeleza kuwa wamefanikiwa kupata boti yenye injini ya (Hos Power 40) kutoka kwa ajili ya kuendeshea doria za udhibiti wa uvuvi haramu yenye uwezo wa kubeba watu 6 na boti hiyo imegarimu kiasi cha Tsh. Milioni 32.9

Pa amesema kuwa kabla ya kupata boti hiyo uvuvi haramu ulikuwa unafanyika hadharani hali iliyopelekea kushindwa kuwakamata watuhumiwa kwa urahisi na wakati mwingine watuhumiwa kukimbia lakini baada ya kupata boti hiyo itasaidia sehemu kubwa kukomesha uvuvi haramu na pia itasaidia kuwakamata hata wanaotorosha na kusafirisha samaki kimagendo.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila ameeleza kuwa Halmashauri tayari imetoa kiasi cha Tsh. Milioni 40 kwa ajili ya kujenga eneo la kuchambulia dagaa na tayari upo mpango wa kuboresha barabara ya kuingia katika soko hilo kwa kiwango cha changarawe.

Naye Afisa Uvuvi wa Wilaya Ndg. Wilfred Tibendelana katika taarifa ameeleza kuwa Halmashauri imeweza kufanya doria 145  na kufanikiwa kukamata zana haramu Kokoro 214, timba 842, nyavu ndogo za makila 655, na nyavu ndogo za dagaa 21 na mitumbwi 92 katuli20 Tupatupa 18 na samaki kilo 5783. Nyavu haramu zilizokamatwa zinakadiliwa kuwa na thamani ya Tsh. Bilioni 2,126,007,500.

Pia ameongeza kwa kusema kuwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 tangu soko la Magarini kurejeshwa kuendelea na shughuli za uzalishaji Halmashauri imeweza kukusanya mapato ya tozo ya ushuru wa samaki dagaa na mazao mengine kiasi cha Tsh. Milioni 113.5na kabla ya soko kufunguliwa Halmashauri ilikuwa,ikikusanya kiasi cha Tsh. 68.5 kwa mwaka.

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa