• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za wafanyakazi |
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya muleba
    • Dira na Dhima
    • Core Values
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara/Vitengo
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Mali asili
      • Ugavi
      • TEHEMA
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utumishi
      • Fedha
      • Mipango na Uchumi
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo/Umwagiliaji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ratiba
  • Madiwani
    • Ratiba
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Vikao vya Mhe.Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
  • Miradi
    • Itakayo- Tekelezwa
      • Inayo-Endelea
      • Iliyo-Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za ofisini au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Makitaba ya Picha
      • gallery

DC NGUVILA AWAHIMIZA WANANCHI KUENDELEA KUITUNZA NA KUILINDA AMANI KATIKA WILAYA YA MULEBA

Imewekwa : July 10th, 2022

Katika harambee iliyofanywa na kanisa Katoliki kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa kanisa la Rulongo, kijiji cha Rwagati, kata ya Kashasha Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhe. Toba Nguvila amewasihi wananchi wa Wilaya ya Muleba kuendelea kuienzi na kuitunza amani kwa maendeleo ya Wilaya na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza wakati wa harambee hiyo, Mhe. Nguvila amewaeleza wananchi kuwa viongozi wa Dini, viongozi wa Serikali na viongozi wa Kimila wanao wajibu wa kuhakikisha wanashirikiana kuzuia vitendo vya uvunjifu wa amani katika maeneo yao.

"Yapo matukio ya kujinyonga na ukatili wa kupiga mtu mpaka kuua, sisi kama viongozi haya mambo ni lazima tuyakemee na sisi kama waumini ni lazima tukemee hizi roho ambazo zinakwenda kinyume na mapenzi ya Mungu" amesema Mhe. Nguvila.

Aidha, amewasihi pia wananchi kuhakikisha wanaachana na tabia ya uuzaji wa kahawa kwa njia ya magendo na kuwasihi kuuza kahawa kwa njia ya mnada ambao itawasaidia wakulima wa zao la kahawa kunufaika na zao hilo.

Sambamba na hayo amewasisitiza wananchi kuhakikisha wanashiriki  ipasavyo katiza zoezi la Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika tarehe 23, Agosti 2022 zoezi ambalo lengo lake ni kuleta maendeleo kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera Mhe. Costansia Buhiye ambaye ndiye alikuwa Mgeni Rasmi katika Harambee hiyo, amewasihi wananchi kuhakikisha wanaimarisha upendo na ushirikiano ili nchi iweze kuwa na amani.

Ujenzi wa Kanisa hilo ulianza rasmi tarehe 8/6/ 2022 ambapo mpaka sasa upo hatua ya msingi ambao umegharimu kiasi cha Tsh. Milioni 6.7 na mpaka kukamilika kwa jengo la kanisa hilo inakadiriwa kugharimu kiasi cha Tsh. Milioni 122.

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,

Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo ya kawaida

  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MSAIDIZI WA HESABU NAFASI MOJA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI III NAFASI SABA November 22, 2023
  • MATOKEO YA USAILI WA NAFASI YA UDEREVA II NAFASI NNE November 22, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA BWENI,UFUNDI NA SHULE MAALUM December 18, 2020
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA MULEBA YASAINI MKATABA WA UJENZI WA SOKO LA KISASA

    January 22, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA KWA KISHINDO TAARIFA ZA HESABU ZA MWISHO ZA MWAKA WA FEDHA 2023/2024.

    September 24, 2024
  • MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BIL 8.1 WILAYANI MULEBA YATEMBELEWA NA KUKAGULIWA NA MBIO ZA MWENGE WA UHURU,2024.

    September 29, 2024
  • MWENGE WA UHURU MKOA WA KAGERA 2024 WAHITIMISHA MBIO ZAKE KATIKA HALAMASHAURI YA MULEBA

    September 30, 2024
  • Angalia zote

Video

Hotuba ya jana ya Rais akiwa nchini Kampala
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ajira
  • Kagera
  • Immigration

Tovuti mashuhuri

  • Ofisi ya Rais TAMISEMI
  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais- UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kagabiro

    Sanduku la Barua: 131 Muleba, Kagera

    Simu: +255 (28) 222-4013

    Simu:

    Barua Pepe: ded@mulebadc.go.tz

Mawasiliano mengineyo

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki@2017 Haki zote zimehifadhiwa